Quantcast
Channel: Lukwangule Entertainment
Viewing all 8662 articles
Browse latest View live

Mkataba wa Gesi umevuja: Tanzania kupoteza shs 1.6 trilioni kwa mwaka

$
0
0


Mkataba wa Gesi umevuja: Tanzania kupoteza shs 1.6 trilioni kwa mwaka
        -       Norway kujirudishia misaada yake yote nchini kupitia mkataba huu

 Zitto Kabwe, Mb
Mkataba wa mgawanyo wa mapato yanayotokana na uzalishaji wa Gesi Asilia (PSA) kati ya Shirika la Mafuta Tanzania na Kampuni ya Mafuta ya Norway umevujishwa (https://onedrive.live.com/view.aspx?cid=0EC42B180C06D0B8&resid=EC42B180C06D0B8%21107&app=WordPdf).TokaMkataba huo uvuje na kuanza mijadala kwenye mitandao ya kijamii, habari zake zimekuwa zinazimwa na hivyo kukosa kabisa mjadala mpana kitaifa na hasa kwa wananchi wenye rasilimali zao. Mwanzoni wengi wetu tulidhani (kwa makosa) kuwa tatizo la mkataba huu ni eneo la umiliki wa kampuni tu (shareholding) kulingana na namna ulivyowasilishwa, kumbe mgawanyo mzima wa mapato unakwenda kinyume na maelezo ya Serikali na TPDC kwa umma.
Mkataba uliovuja unaonyesha kwamba makubaliano ambayo Serikali imeingia na Wawekezaji hawa kutoka Norway yanaenda kinyume kabisa na mfano wa mkataba unaotakiwa kusainiwa (Model PSA). Kwa mujibu wa makala iliyoandikwa na jarida la mtandaoni ( http://africanarguments.org/2014/07/04/leaked-agreement-shows-tanzania-may-not-get-a-good-deal-for-gas-by-ben-taylor/ ) Tanzania itapoteza zaidi ya shilingi 1.6 trilioni kila mwaka kulingana na viwango vya uzalishaji wa gesi asilia katika Kitalu namba 2. Kitalu hiki kinamilikiwa na Kampuni ya StatOil ya Norway na kampuni ya ExxonMobil ya Marekani. Norway ni nchi inayosifika duniani kwa kupambana na rushwa na kwa kutumia vizuri rasilimali yake ya mafuta.
Uchambuzi nilioufanya kulingana na viwango vya mgawo wa mapato kati ya ‘model’ PSA na mkataba huu unaonyesha kwamba Tanzania itapata mgawo kiduchu sana na kinyume na mgawo unavyopaswa kuwa. Mgawanyo ni  kama ifuatavyo katika majedwali hapa chini; Ikumbukwe kuwa mgawanyo huu hupatikana baada ya mwekezaji kuondoa gharama zake za uzalishaji, kinachobakia ndio hugawanywa kati ya mwekezaji na Tanzania.
Jedwali 1 Mkataba wa mgawanyo wa Mapato unaopaswa kutumiwa na TPDC (Model PSA) katika Mikataba na Wawekezaji
Viwango vya uzalishaji kila siku (MMscf per Day)
Mgawo wa TPDC (Profit Gas)

Mgawo wa Mwekezaji (Profit Gas)
0
249.999
50
50
250
499.999
55
45
500
749.999
60
40
750
999.999
65
35
1000
1249.999
70
30
1250
1499.999
75
25
1500
Above 1500
80
20

Jedwali 2 Mkataba wa mgawanyo wa Mapato kati ya TPDC na Statoil/ExxonMobil.
Viwango vya uzalishaji kila siku (MMscf per Day)
Mgawo wa TPDC (Profit Gas)

Mgawo wa Mwekezaji (Share of Profit Gas)
0
299.999
30
70
300
599.999
35
65
600
899.999
37.5
62.5
900
119.999
40
60
1200
1499.999
45
55
1500
Above 1500
50
50

Ukilinganisha majdwali haya utaona kwamba mgawanyo wa mapato utafaidisha zaidi kampuni ya StatOil na ni kinyume kabisa na mkataba unavyopaswa kuwa.
Wakati mgawo wa nusu kwa nusu upo katika uzalishaji wa chini kabisa kwenye ‘model PSA’, kwenye mkataba wa StatOil mgawo huo upo kwenye uzalishaji wa juu kabisa. Ukilinganisha mgawanyo huu wa mapato, iwapo kiwango cha ‘model PSA’ kingetumika Tanzania ingepata shilingi 1.6 trilioni zaidi ya kiwango itakachopata kwenye mkataba wa sasa uliovujishwa. Hii ni kutokana na Bei ambazo Shirika la Fedha la Kimataifa limeweka katika uchambuzi wake (https://www.imf.org/external/pubs/ft/scr/2014/cr14121.pdf) kuhusu Gesi asilia ya Tanzania.
Kwa mujibu wa Mwandishi Ben Taylor katika makala iliyotajwa hapo juu, kiwango cha mapato ambacho Kampuni ya StatOil ya Norway itajipatia kutokana na mkataba huu wa kinyonyaji, katika kipindi cha miaka 15 ya kuzalisha Gesi Asilia nchini itakuwa ni sawa sawa na misaada yote ambayo Tanzania imepata kutoka Norway toka Tanzania ipate uhuru wake mwaka 1961. Tangu Tanzania ipate Uhuru Norway imetoa misaada ya thamani ya $2.5 bilioni, wakati kwa mkataba huu na Kampuni ya StatOil ambayo inamilikiwa na Serikali ya Norway, kwa miaka 15 watapata $5.6 bilioni. Kwa hiyo kwa miaka 7 tu Norway itakuwa imerudisha misaada yote yake mara mbili zaidi!
Kuvuja kwa Mkataba huu kumesaidia sana kuona ukweli wa matamko ya viongozi wetu kuhusu ni namna gani Tanzania itafaidika na utajiri wake wa gesi. Kama kwa mkataba huu mmoja tu Taifa litapoteza matrilioni ya fedha kiasi hiki, ipoje hiyo mikataba mingine 29? Hivi sasa ugunduzi wa Gesi Asilia nchini ni lita za ujazo trilioni 51 ambayo ni sawa na mapipa bilioni 10 ya Mafuta. Katika Gesi Asilia yote iliyopatikana nchini, StatOil peke yao wana jumla ya lita za uzajo trilioni 20, sawa sawa na mapipa ya mafuta bilioni 4 (zaidi ya mafuta yaliyogunduliwa nchini Uganda na Ghana kwa pamoja). Hata hivyo utajiri wote huu utainufaisha zaidi Norway na Marekani kupitia makampuni yao kuliko watu wa Tanzania. Watanzania watabakia wanapewa misaada ya vyandarua na mataifa haya ilhali wanafaidi Gesi Asilia yetu.
Natoa wito kwa Wizara ya Nishati na Madini kutoa tamko kuhusu mkataba huu kati ya Shirika la TPDC na StatOil. Vile vile Kampuni hii ya StatOil kutoka nchi rafiki mkubwa wa Tanzania ina wajibu wa kutoa maelezo ya kina kuhusiana na mkataba huu. Serikali ieleze ni hatua gani inachukua kurekebisha Mkataba huu. StatOil nao waeleze watachukua hatua gani kuhakikisha wanaacha unyonyaji huu mkubwa na wa aibu kwa Taifa la Norway.
Sasa ni wakati mwafaka Watanzania kuweza kuona mikataba yote ya Gesi na Mafuta ambayo Serikali imeingia na Wawekezaji. Uwazi wa Mikataba sasa. Nimewahi kuandika huko nyuma (PRESS RELEASE: Contracts review is a publicity stunt and creation of unnecessary uncertainty in the sector) kwamba njia pekee ya Watanzania kufaidika na utajiri wa rasilimali zao ni kuhimiza uwazi wa Mikataba. Mkataba huu wa StatOil uliovujishwa uwe ni chachu ya kulazimisha Serikali na Makampuni kuweka mikataba yao wazi. Tuanze mashinikizo haya sasa kwa faida ya vizazi vijavyo.


Mbwembwe za mastaa wa bongo, utawapenda

$
0
0
MASTAA  wa bongo waliopata mwaliko kuhudhuria swahili day katika tamasha la nchi za majahazi walionesha vituko vya mwaka ambavyo viliacha wengi wenye utaratibu kujiuliza kulikoni.
Wakati wakichelewa kuingia katuika tamasha, walipofika kitu cha kwanza walitaka kupewa mabodigadi na kuwaacha waandazi wa tamasha hilio katika hali ngumu ya sintofahamu.
Pamoja na kudai walinzi hao maarufu kama mabaunsa kwa kuwa wao ni mstaa na hawataki kudhurika, wengi walionekana kutojua nini hasa kimewapeleka pale kama ni umaarufu au la.
katika ukumbi wa mambo, usiku kila mtu alijua kwamba mastaa wamefika kwani waligeuza eneo hilo kuwa lokesheni kw amabusu na kukaliana.
kituko cha kuklaliana kwa wapenzi hakikulinganisha  na baadhi yao kuonekana kama wanaigiza baada  ya kutaka wapatiwe ulinzi wa kampuni binafsi iliyopewa kazi ya kulinda katika tamasha hilo.
Wasanii hao walisema kwamba wanafuatwa na watu  mbalimbali waliofika eneo hilo wakitaka kupiga nao picha na hivyo usalama wao ni mdogo kitendo.
"Mimi niliona sasa si sawasawa kwani wapo mastaa wengi kutoka Ulaya wapo na hawajahitaji ulinzi wa mabaunsa" alisema ofisa mmoja wa tamasha hilo ambaye alikuwa anashughulika na kupokea wageni na kuwaelekeza wapi kwa kwenda.
Ofisa huyo alisema kwamba Mmoja wa walinzi wa kampuni ya ulinzi iliyokuwa ikilinda eneo hilo ambaye hakutaka kutaja jina lake aliwaeleza  wasanii hao waliotaka ulinzi kwamba kampuni yao haijapewa taarifa za kutoa mlinzi kwa kila msanii wa filamu isipokuwa kazi yao ni kuimarisha ulinzi kwa wote walioudhuria tamasha  hilo.
Kituko kingine ambacho kilielezwa na  ni kitendo cha msanii mmoja kutaka mpenzi wake alipiwe gharama zote kwani ni msanii mwenzake, ingawa huyo mpenzi hakuwa katika orodha ya waalikwa wa ZIFF ambao wanalipiwa gharama  za maisha hapo.
msanii huyo ambaye ni mwangavu na mpenzi wake mwangavu pia ndio waliokuwa wakionekana katika maeneo ya Klabu ya Mambo wakiwa wanapakatana muda wote kama kumbikumbu.
Ilikuwa kazi wakati waandazi walipokuwa wakimweleza kuwa mkataba walioingia ni wa yeye pekee na wala si pamoja na mpenzi wake.

"Kama umemleta wewe ndiwe mwenye jukumu na suala si la kuwa msanii bali nani amealikwa"
 “Hata kama hayupo katika ratiba zenu huyu naye ni msanii naye alipwe gharama kama wasanii wengina,’’ alisema  muigizaji huyo ambaye pia ni dairekta.
 Hata hivyo vituko zaidi vilionekana katika siku ya tuzo ambapo walichelewa kufika na hivyo kulazimika kujichanganya na wengine badala ya maeneo yao ya waalikwa.
Mbwembe za mastaa hao ambazo pia zilionekana katika tamasha kwa kumwaga kilaji na kutokuwa na nidhamu ya kutosha ziklizonekana pia siku ya mkutano na waandishi wa habari, wakifika wakiwa wamechelewa na mmoja wa mastaa ambaye jana yake alitaka mpenzi wake alipiwe alikacha kuhudhuria mkutano huo.
Mkutano huo uliowajumuisha waigizaji, waongoza filamu na wanamuziki kadhaa wa kimataifa, ulikuwa mchungu kwa wasanii ambao walijohi uhalali wa wao kufika mwishoni mwa tamasha huku wakiwapa elimu kuhusu umuhimu wa kuhudhuria matamasha makubwa kama hayo ili kutafuta nafasi za kufanya kazi kimataifa.
 Haji Adamu “Baba Haji” alijibu hoja ya wapi walipokuwepo, swali lililoulizwa na mwandishi kutoka Kenya  alianza kwa kusema: “binafsi nilikuwa na tatizo la kuguza mama yangu huko Tanga ambaye alikuwa anaumwa, sikuweza kuja kwa wakati ili kudadavua maswali yaliyohusu filamu zangu tatu zilizoonyeshwa,” alijitetea.
mwandishi huyo wa kenya alisema lishangazwa sana na jinsiwasanii wa Tanzania walivyoshindwa kuhudhuria japo siku za skrini za filamu zao, hali iliyowamnyima watu kuuliza maswali.
Waandishi waliwashauri kwamba suala la kuigiza na kujifunza na kutafuta fursa ya soko ni muhimu, na hawana sababu za kusubiri mwaliko wa siku moja kwani hauwasaidii kitu.
Maelezo hayo yalitokana na jibu la Richie Richie kwa swali la kwanza kwamba wao hawana fedha za kuhudhuria siku zote kutokana na kutofanya vyema katika biashara.
“Kikubwa kinachotukwamisha tushindwe kuhudhuria tangu siku ya kwanza ni uwezeshaji, filamu za kitanzania jinsi ya uuzaji inashindikana, tungeweza vipi kuishi Zanzibar kwa siku 10, huku filamu tukishamuuzia Mhindi ndiyo imekula kwetu..." alisema na kusema wangelikuwa na fedha wangelikuja kuangalia.
Hali ya ukosefu wa fedha unatokana na wasanii kuwauzia wasambazaji haki zao, ilhali kuna uwezekano wa kumaliza tatizo hilo iwapo wakijituma na kutompa haki zlote msambazaji.
“Ina maana mpaka leo bado hamjajua umuhimu wa elimu? Kuhudhuria katika tamasha hili ni elimu tosha, pia mnakuwa katika nafasi nzuri ya kupata kuhamiana na wasanii wa kimataifa, ni wakati wa kujitambua tumia fedha zako mwenyewe na si kusubiri kuwezeshwa,” alisema mmoja wa waandishi wa habari.
Katika hali inayoonekana kuwa sehemu ya mwendelezo wa mbwembwe za mastaa mmojawapo alimcheka mwenzake alifuata nini chuoni wakati anashindwa kufanya vizuri katikasoko. Kwa Bongo Movie kwenda darasani ni ujinga.
Katika kuonesha tatizo la mastaa wa Bongo hata madairekta waliongiza filamu zao hawakuwepo siku ya tuzo za Kiswahili.
Kwa mfano filamu ya Shahada na dairekta wake Issa Mussa ‘Cloud 112’ walitwaa tuzo za Zuku Bongo Movie katika tamasha la filamu la Zanzibar (ZIFF) huku filamu  ya Shikamoo Mzee ikitwaa tuzo ya wananchi.
Watengeneza sinema hizo wote wawili hawakuwepo Jacob Steven aliondoka siku ile ile asubuhi wakati Cloud hakuwepo kabisa.
Shahada ni filamu ya kidini ambayo inaelezea ni jinsi gani binadamu anapaswa kuishi katika mazingira ya kufuata misingi ya dini.
Filamu ya Shahada imeongozwa  na kuigizwa na Issa Mussa ‘Cloud 112’ wakati shikamoo mzee ilitengenezwa Jacob Steven.
Wakati tuzo za Shahada zilipokelewa na Mtitu, muigizaji shamsa Ford ndiye aliyepokea tuzo ya Shikamoo Mzee.
Aidha katika mlolongo wa tuzo Muigizaji bora wa kiume alikuwa Jackson Kabirigi kupitia sinema ya Kisate na Nguvu ya Imani huku muigizaji bora wa kike akiwa ni Esha Buheti kupitia sinema ya Mimi na Mungu wangu.
mwisho



NAIBU WAZIRI WA MAJI AKIKAGUA TANGI LA MAJI

$
0
0

Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla , ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la
Mvomero  ( wa kwanza kushoto juu ), akijiandaa kuteremka toka  juu ya tangi
la maji safi na salama lililojengwa katika vilima  vilivyopo Tarafa ya
Mlali, wilaya ya Mvomero, mkoani Morogoro , wakati akipofanya ziara ya
kukagua shughuli za miradi ya maji jana katika Kijiji cha Mlali
na Kipera na baadaye kuzindua vituo vya kuchotea maji kwenye vijiji hivyo.

( Picha na John Nditi).

MSTAHIKI MEYA ILALA AFAGILIA METL GROUP

$
0
0
Mtaalamu wa Mkonge kutoka MeTL GROUP, Bw. Iddi Omari (wa kwanza kulia) akimuelezea Mgeni rasmi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (kushoto) aina tofauti za kamba na magunia yanayotengenezwa na kampuni hiyo wakati alipotembelea banda la MeTL GROUP kwenye maonyesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar-es-salaam yanayoendelea  katika viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere,  barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam.



MSTAHIKI Meya wa manispaa ya Ilala, Jerry Silaa ameipongeza makampuni yaliyochini ya Kundi la METL kwa kuhakikisha ajira kwa watanzania na soko la mali ghafi kwa wakulima wa bidhaa mbalimbali nchini.
Silaa alisema hayo leo wakati alipotembelea banda la METL na kujionea bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na makampuni yake mbalimbali  zikiwemo bidhaa za michikichi na katani.
Alisema kwa kutengeneza sabuni, mafuta na mali ghafi nyingine kutokana na michikichi kampuni za Metl zinawezesha wakulima kujiendeleza na pia kuwa na uhakika wa soko.
METL yenye makampuni zaidi ya 25 sehemu kubwa ya bidhaa zake zinatokana na mali ghafi inayozalishwa nchini na nyingine ni zile zinazotumika kwa ajili ya wakulima kama matrekta.
Aidha katika banda hilo kubwa ambapo kulijaa aina mbalimbali ya bidhaa kuanzia sabuni,vitenge, mafuta ya mawese,vinywaji baridi,matrekta na bidhaa za nyumbani, Mstahiki meya huyo alichezesha bahati nasibu za watu waliotembelea banda hilo.
Akizungumzia uwekezaji wa METL, Silaa alisema kwamba anafarijika na jinsi bidhaa za kampuni hizo zinavyoimarika ubora kila mwaka na kusema wakati umefika kwa serikali kuangalia wawekezaji wazawa.
Alisema kwa maoni yake serikali ione jinsi ya kuwasaidia wawekezaji wanaoagiza mitambo toka nje ili kodi wanaoyotakiwa kulipa wailipe baada ya kuanza kazi za uzalishaji.
“Hii itasaidia sana kuwa na wawekezaji wa ndani ambao wataweza kutoa huduma kama soko la mali ghjafi na pia kuongeza thamani ya bidhaa zinazoalishwa kutoka Tanzania” alisema silaa.
Aidha Silaa alipongeza MeTL Group kwa kuweza kutoa ajira kwa watanzania wazawa huku bidhaa zake nyingi zikiwa kimbilio la watanzania wote, hasa wa kipato cha chini.
“Naipongeza MeTL Group, kwa kuzalisha bidhaa bora ambazo ni kimbilio la wananchi wengi… hasa bidhaa zake za mafuta, sabuni, unga, vinywaji na bidhaa zingine kibao” alisema Silaa
Pia aliipongeza MeTL kwa upande wa kutoa ajira na kukuza uchumi hapa nchini, ikiwemo kuzalisha bidhaa nyingi na zenye ubora ikiwemo za kamba ya mkonge ambayo alisema ni majibu ya utunzaji wa mazingira kutokana na vifungashio vya plastiki kuwa chanzo cha uharibifu wa mazingira.
Katika bahati nasibu iliyochezeshwa mkazi wa Kijitonyama Jijiji Dar es Salaam, Irene Manamba amejishindia zawadi ya pikipiki mpya.

Aidha, katika droo hiyo, washindi wengine waliojishindia zawadi mbalimbali katika droo hiyo majina yao na wanakotoka ni  Victoria Charles  ambaye alikuwa mshindi wa pili  mkazi wa Temeke, Julius Kamele (Tabata),  Irene Mushi (Kijitonyama),  Semi Anderson ((Dar es Salaam), Happyness Kalokola (Kitunda), Noel Kalenga (Sinza Kumekucha), Adam  Mkwaya (Mabibo), Mery  Msangi (Dar es Salaam) na Aisha Abeid (Tabata).
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni  ya MeTL GROUP, Fatema Dewji- Jaffer  alieleza kuwa,  droo hiyo ni maalum kwa ajili ya wateja wote waliopata kutembelea  banda hilo tokea siku ya kwanza na kujiorodhesha majina yao.
Fatema alisema MeTL Group imeamua kutoa zawadi  hizo kama shukrani  na kujitangaza zaidi kwa wateja na wananchi waliopata kutembelea na kununua bidhaa  za MeTL Group.
“Kwa ubora wa bidhaa zetu za MeTL Group,  kama  inavyojulikana,  ‘The People’s  Brand’,   kwa droo hii wateja wetu watafurahia  kwa zawadi hizo nono” alisema Fatema.
 Aidha, MeTL Group  imetambulisha rasmi vinywaji  vyake vipya kwenye maonyesho hayo ya Saba Saba, ikiwemo kinywaji kinachopendwa na wengi kwenye maonyesho hayo, MO Cola,  MO Portello na MO Malt.  Vingine ni  MO  Lemon Mint,  MO chungwa na MO Bomba  (Energy  drink).
mwisho

JERRY SILAA ALIVYOTEMBELEA METL GROUP

$
0
0
DSC_0552
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa akiwasili kwenye maonesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar-es-salaam yanayoendelea katika viwanja vya maonesho vya Mwalimu J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar.

DSC_0556
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa akisaini kitabu cha wageni kwenye ofisi za Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania, TANTRADE kwenye viwanja vya maonesho ya Sabasaba mara baada ya kuwasili.

DSC_0571
Afisa Mwandamizi wa TANTRADE, Fidelis Mugenye, (kushoto) akimuonyesha Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa ratiba ya ziara kwenye mabanda mbalimbali ya maonesho ya Sabasaba yanayokaribia kufikia ukingoni.
).
DSC_0574
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa akisalimiana na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa ndani ya ofisi za Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania, TANTRADE.
DSC_0604
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (katikati) akiongozwa na vijana wa skauti kuelekea kwenye mabanda mbalimbali huku akiwa ameambatana na msaidizi wake Anthony William (kushoto).
DSC_0772
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (katikati) akipata maelezo ya sabuni mpya ya MO BEAUTY kutoka kwa Msaidizi wa Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL Group, Kelvin Msangi (kushoto) mara baada ya kuwasili katika banda hilo kwenye maonyesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar-es-salaam yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Meneja Masoko wa MeTL Group, Bw. Aunali Bandali.
DSC_0784
Meneja Masoko wa MeTL Group, Bw. Aunali Bandali akimuonyesha Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaabaadhi za Vitenge na Khanga (hazipo pichani) vinavyozalishwa na kiwanda cha 21st CENTURY Textile Ltd chini ya MeTL GROUP alipotembelea banda la kampuni hiyo kwenye maonesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar-es-salaam yanayoendelea katika viwanja vya maonesho vya Mwalimu J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar.
DSC_0050
Mgeni rasmi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (wa pili kushoto) akipewe maelezo ya ladha za aina tofauti za soda zinazotengenezwa na kampuni hiyo kutoka kwa Msaidizi wa Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL Group, Kelvin Msangi (wa pili kulia) kabla ya droo maalum kwa wateja wanaotembelea banda hilo kwenye maonyesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar-es-salaam yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Meneja Masoko wa MeTL Group, Bw. Aunali Bandali.
DSC_0759
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa akipata maelezo ya sabuni mbali mbali za unga kutoka kwa Mfanyakazi wa Royal Soap Detergent Industries, Aneth Masesa alipotembelea banda la MeTL GROUP kwenye maonyesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar-es-salaam yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam.
DSC_0797
Mgeni rasmi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (kushoto) akipata maelezo ya aina tofauti za kamba na magunia yanayotengenezwa na kampuni hiyo kutoka kwa Mtaalamu wa Mkonge wa MeTL GROUP, Bw. Iddi Omari (wa kwanza kulia) wakati alipotembelea banda la MeTL GROUP kwenye maonyesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar-es-salaam yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam.
DSC_0140
Msimamizi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Bw. Mrisho Millao (kushoto) akichanganya boksi lenye majina ya wateja waliotembelea Banda la kampuni ya MeTL GROUP na kujaza kuponi za kushiriki kwenye droo ya Bahati nasibu ambayo imechezeshwa jana kwenye Maonyesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar-es-salaam yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam. Mgeni rasmi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Slaa (wa pili kulia), Meneja Masoko wa MeTL Group, Bw. Aunali Bandali (kulia) na Msaidizi wa Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya MeTL Group, Kelvin Msangi (wa pili kushoto) wakishuhudia tukio hilo.
MBU_2699
Mgeni rasmi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa, akichagua kuponi ya mshindi wa kwanza kwenye droo kubwa ya Kampuni ya MeTL GROUP kwa wateja waliokuwa wanatembelea banda la kampuni hiyo kwenye maonyesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar-es-salaam yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Meneja Masoko wa MeTL Group, Bw. Aunali Bandali na Kushoto ni Msaidizi wa Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya MeTL Group, Kelvin Msangi.
DSC_0111
Mgeni rasmi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (wa pili kulia) akimtangaza mshindi wa droo maalum kwa wateja wanaotembelea banda la MeTL GROUP kwenye maonyesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar-es-salaam yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam.Na Mshindi huyo ameshinda Zawadi ya Pikipiki aina ya A1 ambayo imesajiliwa na seti mbili ya Vitenge,Wa kwanza kushoto ni msimamizi kutoka Bodi ya Michezo ya Bahatinasibu Bwana Mrisho Millao.Wanaoshuhudia wa pili kushoto ni Msaidizi wa Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL Group, Kelvin Msangi na Meneja Masoko wa MeTL Group, Bw. Aunali Bandali (wa Kwanza kulia).
DSC_0863
Msaidizi wa Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL Group, Kelvin Msangi akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) namna washindi kumi waliopatikana watakavyochukua zawadi zao mara baada ya kupigiwa simu na wahusika kwa ajili ya kukabidhiwa zawadi hizo.
DSC_0191
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (katikati) akipokea zawadi ya soda za MO Cola kutoka kwa Meneja Masoko wa MeTL Group, Bw. Aunali Bandali. Kushoto ni Msaidizi wa Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL Group, Kelvin Msangi.
DSC_0202
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa akiondoka kwenye banda la MeTL GROUP mara baada ya kumaliza shughuli ya kuchezesha droo ya bahati nasibu kwa wateja wanaotembelea banda la MeTL Group kwenye maonesho hayo.
DSC_0728
Mtaalamu wa kutembea juu kamba nchini Hassan Mkenjula a.k.a SPIDERMAN akitoa burudani ya kupiga danadana kwa kutumia mdomo kwenye banda la MeTL GROUP.

WANAHABARI: ANDIKENI HABARI ZA VVU NA UKIMWI ZENYE KULETA MATUMAINI

$
0
0
DSC_0017
Mshauri na Mkufunzi wa Redio Jamii kutoka UNESCO, Bi. Rose Haji Mwalimu akitoa mada inayohusu mchango wa vyombo vya habari katika kuhamasisha matumizi rafiki ya huduma za kuzuia VVU na Huduma za Afya ya Uzazi kwa Vijana wakati warsha ya siku tatu ya mradi mpya kuhamasisha Vijana kuhusu udhibiti wa Maambukizi mapya ya VVU iliyofanyika hivi karibu katika kituo cha Habari na Mawasiliano Sengerema, Mwanza chini ya mradi wa SHUGA unaoendeshwa kwa pamoja na mashirika ya Umoja wa Mataifa UNICEF na UNESCO kwa kuzishirikisha redio jamii nchini.
Na Mwandishi wetu Sengerema
Licha ya jitihada za serikali na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali kupambana na mambukizi ya Virusi Vya Ukimwi hapa nchini, baadhi ya madhehebu ya dini nchini yameelezwa kuchangia kukwamisha juhudi hizo kutokana na imani zao .
Hayo yameelezwa na washiriki wa mafunzo ya siku tatu kwa vyombo vya habari vya jamii Tanzania juu ya kuendesha mradi mpya wa SHUGA unaolenga kutumia vyombo vya habari kutoa elimu na hamasa kwa vijana kukabiliana na maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi.
Washiriki hao kutoka redio mbalimbali za jamii hapa nchini wamesema kuwa kumekuwa na baadhi ya viongozi wa dini ambao kwa namna moja au nyingine hawakubaliani na matumizi ya kondomu kama njia sahihi ya kuzuia sio tu maambukizi ya VVU bali pia magonjwa ya ngono na kama njia ya mpango wa uzazi kutokana na itikadi zao kidini kwa kile wanachokiita kuzuia mimba ni dhambi.
DSC_0025
Pichani juu na chini ni Baadhi ya waandishi wa Habari na Mameneja kutoka vituo mbalimbali vya redio za jamii walioshiriki warsha hiyo wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwasishwa kwenye warsha hiyo.
Yamekuwepo pia madhehebu mengine ambayo yamediriki kuzuia watu wanaoishi na VVU kuachana na matumizi ya dawa za kupunguza makali ya VVU na badala yake maombi ndio njia pekee ya uponyaji jambo ambalo linaonekana kuwa imani potofu kwa sababu ya kuchanganya imani na utaalamu wa kisayansi uliofanyiwa utafiti wa kina na sahihi.
Matokeo yaliyotajwa na washiriki baada ya ushawishi huo wa imani za kidini kwa watu wanaoishi na VVU kuacha matumizi ya dawa zenye kupunguza makali ya virusi ni kudhoofika kwa haraka, kushambuliwa na magonjwa nyemelezi yanayosababishwa na ukosefu wa kinga mwilini na hatimaye kufa.
“Dini ina nguvu kubwa katika kukuza maadili ya kawaida hasa juu ya heshima na utakatifu wa maisha ya binadamu, upendo, huruma na uvumilivu na ina mengi ya kuchangia katika mapambano dhidi ya VVU / UKIMWI hususan huduma za kujitolea na kutoa sadaka kuwasaidia waliopatwa na maambukizi na walioathirika, kuhamasisha watu na makundi mbalimbali kwa kutumia maeneo ya maombi na kuchangisha rasilimali kwa ajili ya kuwajengea vituo vya malezi watoto, wagane na wajane ni muhimu kwa waandishi wa habari kuzitangaza na kuzipa umuhimu wake”.
DSC_0040 
Majadiliano hayo yalitokea baada ya mwezeshaji Bi Rose Haji Mwalimu kuwasilisha mada yake iliyohusu ‘Mchango Wa Vyombo Vya Habari Katika Kuhamasisha Matumizi Rafiki Ya Huduma Za Kuzuia Maambukiziya VVU,’ na kusisitiza kwamba hadi sasa bado hakuna chanjo wala tiba sahihi kutibu VVU na UKIMWI. Njia sahihi ni kuzingatia na kufuata maagizo ya kitaalam katika kuthibiti na kupunguza maambukizi mapya hasa kwa vijana hususan matumizi ya kondomu.
Wakati huo huo waandishi wa habari wamehimizwa kuzingatia maadili na lugha mahsusi katika kuandika habari zinazohusiana na VVU pamoja na watu wanaoishi na VVU na kuacha kuandika habari ambazo zina mwanga mdogo, ni za mfumodume, kejeli, na zinakosa ujumbe mpya.
  DSC_0022Mshauri na Mkufunzi wa Redio Jamii kutoka UNESCO, Bi. Rose Haji Mwalimu akiendelea kuwapiga msasa Mameneja na waandishi wa Habari kutoka redio za jamii zinazoshiriki mradi mpya wa SHUGA.
“Kuna changamoto kubwa katika kuandika na kutayarisha vipindi vya VVU kwa sababu mara nyingi lugha zinazotumika katika taarifa au zinanyanyapaa, kubagua, kuhukumu na kulaumu, vyombo vya habari havitendi haki”, alisema Bi Rose Haji Mwalimu ambaye ni Mshauri na Mkufunzi wa Redio Jamii nchini kutoka UNESCO katika warsha hiyo.
Warsha hiyo ya siku tatu imefanyika katika kituo cha Habari na Mawasiliano Sengerema, Mwanza chini ya mradi wa SHUGA unaoendeshwa kwa pamoja na mashirika ya Umoja wa Mataifa UNICEF na UNESCO kwa kuzishirikisha redio jamii nchini.
DSC_0152Mshiriki wa warsha ya siku tatu ya mradi mpya kuhamasisha Vijana kuhusu udhibiti wa Maambukizi mapya ya VVU ujulikanao kama SHUGA kutoka Sengerema FM Redio, Peter Marlesa (kushoto) na Mshauri na Mkufunzi wa Redio Jamii kutoka UNESCO, Bi. Rose Haji Mwalimu wakifutilia kwa umakini kazi zilizokuwa zikiwasilishwa na vikundi kazi.DSC_0165
Mmoja wa washiriki kutoka redio ya jamii FADECO ya wilayani Karagwe mkoani Kagera akiwasilisha kazi ya kikundi chake ya kutengeneza jedwali la Message Matrix mbele ya washiriki wenzake.
DSC_0030
Afisa Mipango VVU/UKIMWI kutoka UNICEF, Bi. Alice Ijumbe akifuatilia jambo kwa umakini wakati wa warsha hiyo.
DSC_0300
Meneja wa kituo cha Kahama FM Redio, Marco Mipawa (kulia) akimshukuru Mshauri na Mkufunzi wa Redio Jamii kutoka UNESCO, Bi. Rose Haji Mwalimu kwa kuwapiga msasa kupitia mradi wa SHUGA unaolenga kuhamasisha Vijana kuhusu udhibiti wa Maambukizi mapya ya VVU mara baada ya warsha hiyo ya siku tatu.

SHULE YA AWALI YA OJAYS KIDDIES ZONE YAFANYA MAHAFALI

$
0
0
DSC_0401
Watoto wa shule ya Ojays Kiddies Zone iliyopo maeneo ya Kinondoni Block 41, wakiwa kwenye chumba cha mapumziko kabla ya kuanza kwa mahafali ya Kaka na Dada zao wa Laura Class kuanzia miaka 4-5 (T-shrits za kijani) yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Hoteli ya Regency Park jijini Dar mwishoni mwa juma.
DSC_0406
We are happy to Graduate....! Wanafunzi wa Laura Class wakipata Ukodak.
DSC_0640
Mkurugenzi wa Shule yaawali ya Ojays Kiddies Zone iliyopo Kinondoni -Block 41, Bi. Debbie Ndulla akiwakaribisha walezi/wazazi na wageni waalikwa kwenye mahafali ya pili ya shule hiyo yaliyofanyika mwishoni mwa juma jijini Dar.
DSC_0434
Baadhi ya walimu wa madarasa wakitambulishwa kwa wazazi kwenye mahafali hayo.
DSC_0484
Walimu na wanafunzi wa Ojay Kiddies Zone wakitoa burudani kwa wazazi/walezi na waalikwa kwenye sherehe za mahafali hayo.
DSC_0723
Wazazi/walezi wakichukua Ukodak wa watoto wao kwenye mahaali hayo.
DSC_0494
Darasa la awali la Lilies Class wa miaka 1-2 wakitoa burudani ya kuimba kwa wazazi/walezi na wageni waalikwa kwenye mahafali ya kaka na dada zao.
DSC_0595
Mwenyekiti wa Bodi wa shule ya Ojays Kiddies Zone, Bi. Usia Nkhoma Ledama akizungumza na wazazi/walezi kwenye mahafali ya pili ya shule hiyo ambapo aliwashukuru wazazi kwa kuonyesha kuwaamini na kuwapa fursa watoto wao kusoma kwenye shule hiyo yenye maadali bora na kuzingatia ustawi wa mtoto pindi awapo katika mazingira ya shule.
DSC_0623
Mwanaharakati wa Haki za Watoto, Zubeida Masabo akitoa nasaha kwa wazazi/walezi juu ya kuwalinda na haki za msingi ambapo aliwaasa kutenga muda wa kufuatilia maendeleo ya mtoto kila siku, amewashauri wazazi kuwa na taratibu za kutenga muda wa jioni kuzungumza na watoto wao kutokana kukithiri vitendo vya ukatili dhidi ya watoto hali itakayosaidia kubaini vitendo vya uovu.
DSC_0619
Mmoja wa wazazi Dr. Isaac Maro akifafanua jambo kwa wazazi/walezi likiwemo suala la afya kwa watoto hasa magonjwa ambukizi kama Tetekuangua (chicken pox) ambapo wazazi wengi wamekuwa na hofu endapo kunatokea mlipuko wa ugonjwa huo kwenye mazingira ya shule wasihofu na kushauri watoto kuendelea kuhudhuria masomo kwani wakiumwa utotoni ni nafuu zaidi kutibika kuliko kuugua ukubwani.
DSC_0502
Watoto wa Lantana Class kuanzia miaka 3-4 wa shule ya awali ya Ojays Kiddies Zone wakijitambulisha mbele ya wazazi/walezi kwenye mahafali hayo.
DSC_0534
Kwa picha zaidi bofya hapa

HABARILEO DAKAWA ... KUPIGA CHABO INARUHUSIWA .

$
0
0

Baadhi ya Wakazi Kata ya  Dakawa, Wilaya ya Mvomero, Mkoani Morogoro,wakipitisha macho yao kwa mali ya tajiri wangu gazeti la HABARILEO wakati wakisubiri  kuanza kwa  mkutano wa hadhara wa Mbunge wa Jimbo la Mvomero, Amos Makalla ( haonekani pichani) , ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maji.( Picha na John Nditi).




TASWA AIPS mafunzo

$
0
0


Habari wadau, Chama cha Kimataifa cha Waandishi wa Habari za Michezo (AIPS), kimeandaa mafunzo kwa ajili ya waandishi wa habari za michezo chipukizi wa umri kati ya miaka 19-25 yatakayofanyika Doha Qatar mwishoni mwa mwaka huu wakati wa mashindano ya Dunia ya Mchezo wa Kuogelea.

Kutokana na hali hiyo, AIPS imetoa nafasi chache kwa watakaokidhi vigezo vyao katika mabara mbalimbali duniani. Hivyo nimeattach barua yao na nini kinatakiwa katika mafunzo hayo, ambayo wahusika watagharamia nauli ya kwenda Doha na kurudi mji husika anaotoka mhusika, chakula na malazi muda wote atakaokuwa huko.

Kwa vile hatua ya mwisho itahusisha chama cha nchi husika kumthibitisha muombaji, naomba wote watakaofikiri wana sifa zinazotakiwa wasome vizuri hiyo attachment, kisha watume kwa Makamu Mwenyekiti TASWA, Egbert Mkoko ambaye ndiye atasimamia jambo hilo kwa email: njali5@yahoo.com na taswatz@yahoo.com

Lakini pia kama utamudu unaweza ukaomba binafsi bila kutumia chama na mwisho wa kufanya hivyo ni Agosti 15 mwaka huu na watume kwa email:youngreporters@aipsmedia.com. Kwa watakaotaka kupitia TASWA wajitahidi kabla ya Agosti 10 mwaka huu.

Tusihofie kuomba kwani mwaka 2011 aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Mtanzania mwenzetu, Mwita Mwaikenda aliomba nafasi hiyo na aliipata. Ukiwa unahitaji ufafanuzi tuwasiliane 0713-415346.

Nawasilisha,
Katibu Mkuu TASWA

Airtel yamwagia wahariri vifaa vya michezo

$
0
0

Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando akimkabithi Nahodha wa timu ya wahariri  Bwana Kulwa Karedia ,  vifaa vya michezo kwaajili ya mechi kati ya timu ya Jukwaa la wahariri na timu ya waandishi wa mkoa wa Mtwara itakayofanyika siku ya Ijumaa tarehe 11 Julai mkoani Mtwara Airtel yamwagia wahariri vifaa vya michezo

KAMPUNI ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania imetoa msaada wa vifaa vya michezo wenye thamani ya Sh milioni 1.1 kwa timu ya Jukwaa la  Wahariri Tanzania (TEF).
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana, Ofisa Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando alisema uamuzi wa kutoa msaada huo umefikiwa kutokana na kutambua mchango wa vyombo vya Habari nchini.
“Tunafaurahi kuwaambia kwamba leo (jana),tunakabidhi msaada wa vifaa vya michezo ndugu zetu wahariri ambao wanajiandaa na mchezo wa kirafiki mkoani Mtwara Jumamosi hii.
“Kama kwa vile wahariri ni watu ambao wanakuwa na majukumu mengi ya kila siku kwenye vyumba vya Habari, tunaamini baada ya mkutano wao, watapata fursa ya kucheza mchezo wa soka pale Mtwara ili kuweka miili yao sawa,”alisema Mmbando.
Baadhi ya vifaa vilivyotolewa ni pamoja na jezi seti moja,mipira mitano, filimbi tatu,fulana na traksuti tano.
“Hii ni sehemu tu ya msaada mdogo,tunategemea vitawasaidia jamaa zetu kuonyesha makekeo yao,”alisema Mmbando.
Akipokea msaada huo, Nahodha wa timu ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Kulwa Karedia aliishukuru Airtel kwa msaada huo na kusema umekuja wakati mzuri.
“Unajua mawasiliano bila waandishi wa habari hayapo, nadhani ndiyo maana Airtel wameona umuhimu wa kutoa msaada huu na sisi tunasema hatutawaangusha,”alisema Karedia.
Alisema timu yake inatarajia kuondoka kesho kuelekea Mtwara ambako Jumamosi hii watacheza na timu ya waandishi wa habari mkoa wa Mtwara.
Kikosi  cha TEF kinaundwa na wachezaji kama Theopil Makunga,Revocatus Makaranga,Jesse Kwayu,Manyerere Jackton,Ansbert Ngurumo,Salehe Mohamed,Neville Meena,Mnaku Mbani,Salim Said Salim, Wallace Maugo na Erick Anthony ‘Chinga’.
Mwisho

Lowassa amtaka Aveva kutolipiza kisasi Simba

$
0
0


Waziri mkuu wa zamani na mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa ameutaka uongozi mpya wa Simba kutolipiza kisasi au kufukua maovu ya uongozi uliyopita na badala yake kujikita katika kuweka mikakati ya kuendeleza klabu.

Lowassa alisema hayo ofisini kwake jijini dar es salaam jana alipotembelewa na Rais mpya wa Simba Evans Aveva.

Lowassa amemtaka Aveva kuunganisha wanachama wa Simba kwa manufaa ya Soka la Tanzania.

Aidha aliwataka viongozi wa vilabu vikubwa nchini kusajili zaidi wachezaji wa nyumbani na kuachana na tabia ya kukimbilia kusajili wachezaji wa kigeni kwani hiyo inadhoofisha uimara wa timu ya taifa.

Lowassa alitolea mfano timu ya taifa ya Uingereza ilivyofanya vibaya katika Kombe la dunia akisema inatokana na vilabu vya ligi Kuu ya nchi hiyo kuwa na wachezaji wengi wa kigeni kuliko wale wa ndani.

Kwa upande wake  Rais huyo wa Simba Aveva alisema uongozi wake umejipanga kuwekeza katika Vijana ili kupunguza gharama za kusajili wachezaji wapya kila msimu.

Pia alimueleza Mh Lowassa kuwa wanatarajia kufungua hosteli katika kipindi kifupi kijacho katika eneo jipya la klabu hiyo huko Bunju.

Amesema awamu ya pili ndiyo itakuwa ya ujenzi wa uwanja ambapo alimuomba Mh Lowassa kukubali mualiko wa kufanya harambee ya kukusanya fedha za ujenzi wa uwanja huo wakati ukifika.

TAARIFA YA KISOMO CHA AROBAINI YA IRAK HUDU

$
0
0


TAARIFA YA KISOMO CHA   AROBAINI YA  NDUGU YETU
                                MAREHEMU(Bondia) IRAKI  HUDU(RIP)

Ndugu wanajumuiya, mabibi na mabwana
Familia ya marehemu (Bondia)  Iraki Hudu,inapenda kuwajulisha maadhimisho ya arobaini ya marehemu Iraq Hudu itayofanyika siku ya 19 Julai 2014 Shughuli hii itafanyika jioni
wakati kufutari nyumbani kwa marehem huko Buguruni ,Rozana,Dar-es-salaam .

Shughuli hii ya arobaini kwa kuwa imengia katika mwezi mtukufu wa mfungo wa Ramadhan,familia ya marehem imeamua kutimiza shughuli hii kwa kufuturisha na
kisomo.

 Kwa heshima na taazima tunawaomba ndugu na jamaaa wote kushiriki katika shughuli hii. Marehemu Iraq, alitutoka tarehe 13.Juni 2014na kuzikwa siku ya 14.Juni 2014 Hivyo hatunabudi kutekeleza wito huu wa kuadhimisha siku ya kisomo chake. Kwa maelezo na habari zaidi, unaweza kuwasiliana na ndugu (Mtoto) wa marehemu kupitia simu hii 0717795070 kwa wanaopiga kutoka nje ya nchi +255 717795070
Asanteni sana.
Wenu, mwakilishi wa familia ya marehemu  Dani Huddu.

abiria wa TRL wasafirishwa kwa mabasi

$
0
0
Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania – TRL unawaarifu wananchi kwa jumla kuwa imefanikiwa kuwasafirisha kuja Dar abiria takriban 678 waliokwama katika Stesheni ya Manyoni baada ya njia kuharibiwa na ajali ya treni ya mizigo.

 Zoezi hilo linaloendeshwa kwa awamu mbili tofauti lilianza usiku wa manane hadi saa 10 usiku wa kuamkia leo .
Kwa mujibu wa taarifa ya uongozi zoezi la pili litaanza tena kuanzia saa asubuhi ya leo kwa abiria wapatao 699 waliosalia kutegemeana na kupatikana mabasi mengine zaidi ya 11 yanayohitajika.
Kukwama kwa treni hiyo iliyokuwa ikitokea Tabora kuja Dar kumesababishwa na ajali ya treni ya mzigo iliyokuwa ikienda Bara ambapo ilitokea kati ya Stesheni za Kintinku na Makotopora km 539/6-0 jana saa 6:50 mchana. Katika ajali hiyo mabehewa 7 yalianguka na moja liliacha reli.
Tathmini ya Wahandisi wetu ni kuwa kazi ya kukarabati njia itachukua saa 12 na hivyo njia inatarajiwa kufunguli wa saa 6 usiku wa manane leo.
Safari ya abiria kwenda bara ya leo Julai 08, 2014 itaendelea kama ilivyopangwa hata hivyo muda wa kuondoka umesogezwa mbele ambapo itaondoka stesheni  ya Dar es Salaam saa 2:30 usiku.

Imetolewa na Ofisi ya Uhusianokwaniaba ya MkurugenziMtendajiMhandisiKipallo Aman Kisamfu.
TRL MakaoMakuu,
Dar es Salaam.
Julai 08, 2014

Baraza la Nne la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu klazindua mfumo wa malalamiko

$
0
0
Mgeni rasmi Baraza la Nne la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu,Waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya Salum (Mb) akiwaonesha wajumbe wa  mkutano huo kitabu cha Mfumo wa Kushughulikia Malalamiko ulioandaliwa na Ofisi hiyo mara baada ya kuuzindua leo katika kikao cha kwanza cha Baraza hilo mkoani Tanga. Katikati ni Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Zanzibar Mohamed Hafidh Rajab na kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa.

Maringo ya ZIFF na mahaba ya sinema

$
0
0

HAPANA shaka kabisa kwamba tamasha la mwaka huu lilikuwa na mafanikio makubwa kutokana na aina ya ushiriki wa sinema na waliohudhuria ambao walifanya mambo ambayo hayakutegemewa.
Ndiyo, hayakutegemewa kutokana na ukweli kuwa mara nyingi tamasha la nchi za majahazi  linakuwa na changamoto nyingi ambazo nyingi zao ni mabadiliko ya dakika mwisho.
Kutotegemewa huko ndiko kulikofanya tamasha hili lenye dhima kubwa ya kuutangaza utamaduni wa sinema likipita miaka 17 kwa mbwembwe ya mafa nikio.
Katika mazungumzo yangu na Meneja wa Tamasha, Daniel Nyalusi,katika hoteli ya Double Tree by Hilton, alisema kwamba kwa maoni yake tamasha la mwaka huu limekidhi nia na kiu ya waandazi hasa kuleta mafunzo ya uandishi wa skripti na utengenezaji wa sinema.
“Tuna matatizo makubwa sana ya utengenezaji wa skripti na bila kuwa na skripti bora huwezi  kutengeneza sinema bora” alisema Nyalusi na kuongeza kuwa kuletwa kwa Mitchell Peck (Projuza wa Hollywood) na Nick Broomfield ni neema kwa walioamua kujifunza.
Katika mtazamo wa kawaida unaweza kuona kwamba kulikuwa na watu wachache lakini tamasha la filamu ambalo mwelekeo wake si muziki kuwa na watengeneza filamu 40 kutoka nchi tofauti 12 zenye kiwango tofauti cha maendeleo ni Baraka kubwa.
Ndio maana wakati Profesa Martin mhando, ambaye ni Mtendaji wa ZIFF akifungua tamasha hilo alikuwa na kila aina ya majivuno akiwa na uhakika kwamba mafanikio ya mwaka huu yanaleta mafanikio mebngine kwa tamasha la mwakani ambalo litafanyika mara tu baada ya kumalizikwa kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani  Julai 18 – 26, 2015 likiwa na moto wa Mawimbi na Njozi za Tumaini.
Kwa miaka 17 tamasha hili kubwa lenye shughuli nyingi za kifasihi na sanaa halijaweza kutumika vyema na watanzania ambao ama kwa woga au kwa sababu ya nabii kutopendwa nyumbani kwake wamewaachia wageni kulitumia kupanda ngazi.
Kama lilivyofunguliwa kwa maandamano ya kupinga ukatili hapo Juni 14 ambapo maandamano hayo yalipokewa Ngome Kongwe , zilifuata siku zenye mahaba makubwa na sinema ambapo kwa siku mbili filamu zaidi ya 40 zilikuwa zimeoneshwa.
 Filamu zilizoingia katika mashindano zilikuwa 80, huku filamu za Kiswahili kwa upande wake  katika Swahili Movie zilikuwa 23 na filamu nyingine zilikuwa tamthilia ambazo zilikuwa na saa kadhaa kibindoni.
Pengine ni kutokana na kukosekana kwa fedha za kuwawezesha kukaa Ngome Kongwe na kujifunza na kutafuta soko filamu, lakini filamu zilizooneshwa zilikuwa na  nguvu kubwa kiasi ya kwamba kuzikosa ilikuwa ni tatizo kubwa.
Pamoja na kuwepo na kanuni za bodi ya sensa, bado sinema zilikuwa na ukakasi ule unaotakiwa katika kuivua na kuiangalia jamii.
Mathalani kulikuwa na sinema Mother of George, filamu iliyokuwa inajadili kwa kina kabisa tatizo la uzazi kwa mwanaume. Filamu hii ilimezwa na sense na kuwafanya waliofika kuiangalia kupiga kelele kila mara.
Profesa Martin Mhando alisema kwamba tamasha la mwaka huu limetulia, ingawa lina hekaheka zake ambazo hakuwa tayari kuzizungumza zaidi ya kusema anaona kuna mafanikio makubwa.
Pamoja na mafanikio yanayoelezwa kitaalamu bado wananchi waliopata nafasi ya kuzungumza walielezea kutofurahishwa na baadhi ya mambo hasa utangazaji wa tamasha.
Aidha baadhi ya wafanyakazi wa mTamasha hilo walilalamikia serikali kutokuwa na  mkono katika tamasha hilo, kutokana na kulidai fedha wakati wenyewe hawalipigii chapua kama moja ya matamasha yanayoweza kuingiza fedha kupitia watalii wanaokuja kuangalia sinema.
Pamoja na ukweli kuwa watengeneza sinema kama akina David Cecil (Uganda / Uingereza) aliyetengeneza Bye Bye Mzungu, Richard Pakleppa (Namibia)  aliyetengeneza  A Taste of Rain, Hughes Gentillon (Haiti)  aliyetengeneza  Love Me Haiti, Sean Hodgkinson (Trinidad & Tobego)  aliyetengeneza A Story About Wendy 2 walikuwepo kwa majadiliano na watanzania, watanzania watengeneza sinema hawakuwepo zaidi ya waandishi wa habari.
Aidha muigizaji wa Afrika Kusini Terry Pheto ambaye alielezea nia yake ya kujifunza Kiswahili kuweza kufanyakazi na watu wa Afrika Mashariki hapakuwepo na mtu ambaye angelichukua anuani yake kati ya wale wanaoendesha Bongo au Swahili movies ili kutanua maarifa na uwezo.
Said Mmanga mmoja wa mashabiki wa safu ya sinema ya gazeti hili amesema katika mchango wake kwamba shida kubwa inayowakabili watanzania ni kutojua namna ya kupata elimu ambayo inasaidia katika kazi zako.
“ni ngumu kwenda kujiunga na chuo cha utengenezaji sinema, ni ngumu kwenda mbali kwa matamasha kuuza kazi, lakini ugumu unatoka wapi kama unaletewa walimu na soko ubavuni kwako” aliuliza na kuongeza kwamba watengeneza sinema wa Tanzania hawajawa mastaa wa kutosha kutojifunza ktuoka kwa wengine.
Pheto, ambaye alishacheza sinema zilizompatia tuzo na ya mwisho kama mke wa kwanza wa Mandela katika filamu ya Mandela: Long Walk to Freedom hakuwa tu ameeleza kufurahishwa kwake kufika Zanzibar lakini alitamani  kufanya kazi ya kutengeneza masimulizi ya kiafrika kwa kutumika kwa waafrika wenyewe.
Hata mtu hakuweza kuhudhuria kozi lakini angeliweza kujifunza kitu , kuongeza mtanadao na pia kuangalia watu kama  MAISHA Film lab wanafanya nini kwani kwa mara ya kwanza mwaka huu walikuwa na somo la kutengeneza sinema tena kwa lugha ya Kiswahili na mastaa wa bongo movies hawakuomba.
Katika masuala ya muziki kitu ambacho kinaambatana sana na sinema kwani ni sehemu ya sinema ukiachia mbali kutofika kwa J Martin bado  kulikuwa na muziki wa kutosha kutoka kwa Malawi’s Body, Mind & Soul, DJ Kaka Kahlil kutoka Puetro Rica/  marekani walitia fleva katika muziki wa Tanzania ambapo akina Ras Inno, Grace matata kuwataja kwa uchache walifanya shoo za nguvu.
Katika mahojiano na waandishi wa habari wanamuziki wa Tanzania walitaka sinema za Tanzania kutumia vifereji vya sauti kutoka nchini badala ya kuiba kutoka nje.
Ni dhahiri katika sinema kuanzia ile iliyofungua pazia hadi ya mwisho kulikuwa na makubwa katika tamasha la filamu hasa ubora wa sinema zilizoingia mwaka huu.
Huwezi kwa namna yoyote ile ukadharau filamu ya Mandela au filamu ya half of a yellow Sun, King’s Virgin, A taste of Rain, Mother of George White Shadow na Thorn  of the Rose kuzitaja kw auchache.
Hakika ni mahaba ya sinema na maringo ya ZIFF kwa kuwezesha tamasha hili kwa miaka mingine tena.
mwisho

Brazil, yatwangwa, yapondwa yachanganyikiwa 7-1

$
0
0


HUWEZI  kuamini lakini ni kweli kuwa Brazil, taifa linalolala, kula na kuamka na soka limepata aibu ya mwaka baada ya kushushiwa kipigo cha paka mwizi na Ujerumani kiasi cha kutoka uwanjani na kapu la magoli ambalo halijawahi kuonekana katika siku za karibuni kwenye fainali za Kombe la Dunia la FIFA.
CNN wakielezea kipigo hicho cha paka mwizi walisema : kwanza hakuna aliyeamini.Kisha machozi yakatiririka kwa uchungu.
Kisha wakaendelea: wakiwa wamepigika, kuumizwa na kujeruhiwa vibaya ndoto za kombe la dunia kwa upande wa Brazil zimeota mbawa.
Wakaendelea kuandika:
Ni matokeo ambayo yanaonekana kwa muda mrefu ujao yatawaganda na hawataelewa kwa taifa ambalo linaaminika na linajiamini kwamba wao ndio soka.
Kisha wakaandika:
Brazil, unbeaten in a competitive fixture at home since 1975, had been on their way to heaven, according to their manager Luis Felipe Scolari, as they sought a sixth world crown.
Ninety minutes later Scolari, his players, and their millions of fans must have thought they had tumbled into Dante's Inferno.
They had congregated in Belo Horizonte -- the scene of Brazil's last competitive defeat on home soil -- to roar their team into Sunday's final in Rio de Janeiro.
But nobody had told Germany as the European side produced a performance which was as staggering as the result.
A 7-1 defeat almost flattered Brazil given its dire showing.
Outplayed, outfought, outthought -- if this was a boxing match it would have been stopped long before the halftime whistle.
And yet, this had been coming.
There are few who would have expected the punishment to be so severe, but those in yellow who had kicked and dived their way around the field over the past few weeks were never likely to succeed in the long term.
Let there be no doubt -- there is and was nothing beautiful about this Brazilian side.
Jogo Bonito is just a sepia toned memory -- like a teenage fling or a summer romance.
This Brazil side is like an errant school child who plays up as often as possible until somebody steps forward to put it back in its place.
That petulance was quickly displayed as Marcelo claimed an early penalty after an impeccably timed Philipp Lahm tackle.
Occasionally the errant child gets a helping hand, as it did in its opening game against Croatia or during its quarterfinal victory over Colombia.
But what Brazil and its carefree kids had not bargained for was that one teacher who petrifies everybody and chills students to the bone.
You know the teacher -- the one that doesn't even need to speak to get his or her message across when just an ice cold stare will suffice.
The teacher who can cause nightmares and bring out cold sweats with just a glance is the one which turned up in Belo Horizonte with the name of Germany displayed proudly upon its shirt.
This was the day Brazil was taught a lesson -- and what a painful lesson it was as Germany provided a stark reminder of just how far those in yellow have fallen.
There isn't a detention long enough for those who produced Brazil's most insipid performances in World Cup history and the heaviest defeat in the country's history.
Five times has Brazil held the World Cup trophy aloft -- but this current generation does not come close in comparison to any of those which have been successful in years past.
Would it have been different had Brazil's star player Neymar been there?
Since the golden boy of Brazilian football was taken off on a stretcher during the quarterfinal win over Colombia, the country has been plunged into misery.
His back injury, sustained following a poor challenge by Colombia's Carlos Zuniga, didn't just damage his vertebrae -- it shattered the hopes and dreams of a nation consumed by the ideal of winning.
Every single waking moment has been spent discussing the absence of Neymar, the man who has scored 35 goals in 54 appearances.
His goals have propelled an average side to heights that it surely never would have reached without him.
But even his presence would only have delayed the inevitable, insisted Brazil's coach.
"This would have happened even with Neymar," said Scolari.
"If Neymar were in there things would not have been much different. He is a striker, don't forget that.
"Germany was able to take control of the game early on. The result has nothing to do with the anthem, the emotions, or Neymar.
"It wouldn't have mattered if Neymar was in the pitch. We're not going to make excuses for what happened."
Arguably it was the suspension of captain Thiago Silva which really sealed the host nation's fate.
One of the finest central defenders in the game, Silva has not only shielded his side's goal, he has provided the leadership that this team relies on.
For many of the players, the emotion of the occasion and the pressure that has gone with it has often appeared to leave them overwhelmed.
"The blame for this catastrophic result can be shared between us all, but the person who decided the line-up, the tactics was me. It was my choice," Scolari, who led Brazil to glory in 2002, told reporters.
"We tried to do what we could, we did our best - but we came up against a great German team. We couldn't react to going behind.
"Not even the Germans can tell you how this happened -- but it's because of their skills and you have to respect that.
"My message for the Brazilian people is this: Please excuse us for this performance. I'm sorry that we weren't able to get to the final -- and we're going to try to win the third place match. We still have something to play for."
For Brazil this World Cup was not just about victory -- it was about exorcizing the demons of 64 years ago, demons which have haunted a nation in a merciless fashion.
In 1950 it was Uruguay that ransacked the Maracana stadium in Rio and brought Brazil to its knees.
Those players were never allowed to forget what had come to pass, but at least now, their transgressions may be temporarily forgotten.
This current generation has grown up with the knowledge it would have the opportunity to avenge that day -- instead it wrote a new chapter of humiliation into the history of Brazilian football.
From the very moment Germany opened the scoring through Thomas Muller in the 11th minute, Brazil's world began to unravel.
This was not just a beating. This was a merciless destruction, not just of a football team but of a nation's football heritage.
Within 18 first half minutes, Germany had delivered a barrage so deadly that Brazil never stood a chance of recovering.
Miroslav Klose became the World Cup's all-time leading scorer with 16 when he netted his side's second goal, firing home the rebound after Julio Cesar had saved his initial effort.
A minute later it was 3-0 -- Toni Kroos thumping home from the edge of the penalty area as Brazil imploded.
With Brazil floored, Germany's ruthless streak came to the fore with Kroos adding his second after a one-two with Sami Khedira.
Germany's players didn't know whether to celebrate or laugh -- in the end, they didn't even celebrate given the embarrassing ease with which they scored.
It was Khedira who made it five, finishing coolly after a neat interplay with Mesut Ozil to leave Scolari's men decimated.
Booed off at the interval, there was little to cheer about in the second half with substitute Andre Schurrle's 69th minute strike rubbing salt in Brazilian wounds.
As Brazilian fans began to leave Estádio Mineirão in Belo Horizonte, Schurrle netted a spectacular seventh to inflict the nation's heaviest ever defeat.
Oscar's late effort reduced the deficit to a mere six, but not even he could bring himself to celebrate such was the embarrassment.
The final whistle brought relief -- not just for those in yellow on the pitch but for those who had suffered with them on the field.
While Germany celebrated reaching the final for the first time since 2002, Brazil's player were left inconsolable with grief.
Tears flowed, heads were bowed but perhaps in time those players will come to realize that they were simply not good enough.
For Brazil, it is a lesson learned. For Germany, it is the latest chapter in what could be a glorious story.
"We need to stay humble," said Germany coach Joachim Low. "We have to stay concentrated until Sunday.
"We're obviously going to celebrate a bit but we have to start focusing right away on the next match.
"But I'm not worried about that," added Low. "The players all have their feet firmly on the ground and they won't let this win go to their heads."
Argentina and the Netherlands -- you have been warned.
Pole sana wapenzi wa Brazil ile haikuwa kawaida!!!

LIGI SOKA YA KUPAMBANA NA UJANGILI YAZINDULIWA IRINGA

$
0
0

Timu ya Idodi FC na Kitisi FC zinazoshiriki mashindano ya kombe la SPANEST linaloenga kuwahamasisha vijana kushiriki katika vita ya ujangili wakiingia uwanjani

MASHINDANO ya  ligi soka kuwania Kombe la SPANEST yamezinduliwa juzi na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk Christine Ishengoma katika mchezo uliozikutanisha timu ya Idodi FC  na Kitisi FC katika uwanja wa Shule ya Msingi Idodi.

SPANEST ni mradi wa Kuboresha Mtandao wa Hifadhi Zilizo Kusini mwa Tanzania ambao kwa kushirikiana na Hifadhi ya Taifa ya Ruaha ndio walioandaa  mashindano hayo.

Mbele ya mashabiki wao zaidi ya 1,000 wenyeji Idodi FC waliutumia vyema uwanja wao wa nyumbani na kufanikiwa kuibuka vinara kwa kuichabanga Kitisi FC kwa mabao 2-0.

Bao la kwanza la Idodi FC lilipatikana Dk 23 ya mchezo kupitia kiungo wake mkabaji Same Gembe aliyopokea pasi safi kutoka kwa mshambuliaji wao  Maneno Fumbe na kufanikiwa kupiga shuti kali lililomshinda golikipa wa Kitisi FC, Maneno Ng’ingo.

Kipindi cha kwanza kilimalizika kwa Idodi FC kuwa mbele kwa 1-0 bila dhidi ya Kitisi FC walioonekana wachovu muda wote wa mchezo.

Katika kipindi cha pili cha mchezo, Idodi FC waliongeza kasi na katika Dk 55 ya mchezo walifanikiwa kuongeza bao la pili lililofungwa kupitia kiungo mshambuliaji, Amad Kambangwa.

Kuzamishwa kwa bao la pili kuliwafanya wapinzani wao wapoteane zaidi na mpaka kipenga cha mwisho cha mchezo huo kinapulizwa, Kitisi FC walikuwa wamelala kwa bao 2-0.

Idodi FC katika picha

Kitisi FC katika picha
Akizindua mashindano hayo yatakayozikutanisha timu 21 kutoka vijiji 21 vinavyozunguka hifadhi ya Taifa ya Ruaha, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk Ishengoma alisema ikiendelezwa ligi hiyo itaongeza mwitikio wa vijana katika harakati za serikali na wadau wake za kupambana na ujangili.

Alisema vijana kama sehemu muhimu ya jamii wana nafasi kubwa ya kufanikisha mapambano dhidi ya ujangili na akawataka wadau wote kuwashirikisha ili kufanikisha kampeni za uhifadhi wa wanyamapori.

Mratibu wa  SPANEST, Godwell Olle Meing’ataki alisema lengo la ligi hiyo yenye kauli mbiu “Piga Vita Ujangili Piga Mpira Okoa Tembo” ni kuwaunganisha vijana katika vita dhidi ya ujangili wa wanyamapori wakiwemo Tembo.

Alisema wazo la kuunganisha vijana katika vita ya ujangili linaonekana kuwa njia muafaka ya kutokomeza ujangili kutokana na ukweli kwamba vijana ndiyo walengwa wakubwa katika kushawishika kuingia kwenye maeneo yaliyohifadhiwa na kufanya ujangili.

“Takwimu za ujangili katika maeneo yaliyohifadhiwa zinaonesha kuwa vijana wengi hukamatwa katika matukio hayo. Vijana hao hurubuniwa na watu wenye fedha ili wafanye ujangili,” alisema.

Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Iringa Vijijini (IRFA), Juma Lalika alisema ligi hiyo inayakutanisha makundi sita. Kila kundi linaundwa na timu mbili hadi nne.

Alisema washindi nane kutoka katika makundi hayo yanayoundwa na tarafa za Idodi na Pawaga, wataingia robo fainali.

Kwa mujibu wa Mratibu wa SPANEST, mshindi wa kwanza atapata kikombe, medali ya dhahabu, seti moja ya jezi, cheti, Sh 300,000, kutembelea Hifadhi ya Ruaha.

Mshindi wa pili atapata medali ya fedha, mipira 2, cheti na Sh 200,000 taslim huku mshindi wa Tatu akipata medali ya shaba, cheti na Sh 100,00 huku mshindi wa nne akipta Sh 50,000 katika ligi hiyo itakayomalizika Agosti 8, mwaka huu.

SERIKALI YATENGA SH. BILION 21 KUMALIZA TATIZO LA VITABU

$
0
0


RAIS Jakaya Kikwete amesema serikali imetenga kiasi cha sh. Bilioni 21 katika bajeti ya mwaka wa fedha wa 2014/2015 kwa ajili ya kumaliza tatizo la upungufu wa vitabu kwenye shule za sekondari.

Kauli hiyo ameitoa wakati akihutubia wananchi wa kata ya Kimbe baada ya kuweka jiwe la msingi kwenye maabara ya masomo ya sayansi ya sekondari ya kata hiyo ambapo ujenzi wake utagharimu jumla ya sh. Milioni 135 hadi kukamilika.

Mpaka sasa ujenzi wa maabara hiyo ya masomo ya Fizikia, Kemia na Baiologia ulioanza mwaka jana umegharimu jumla ya sh milioni 59 ambapo kati ya hizo mchango wa wananchi ni sh. Milioni 47.4, halmashauri sh milioni 12.5 na kiasi kilichobaki ni mchango wa serikali kuu ambapo ujenzi huo uunatarajiwa kukamilika baadae mwezi Novemba mwaka huu.

Amesema fedha hizo zimeongezwa ili kuendea kukabiliana na uhaba wa vitabu vikiwemo vya mazomo ya Baiolojia, Kemia, Fizikia na Hisabati ili kuwawezesha wanafunzi wanaosoma katika shule za sekondari hususan za Kata kujifunza masomo ya sayansi.

RAIS AKIMBIZWA AFRIKA KUSINI KWA KUTAPIKA

$
0
0


RAIS Michael Sata ambaye Jumapili iliyopita alisherehekea miaka 77 ya kuzaliwa kwake leo anatarajiwa kwenda Afrika Kusini kwa matibabu.
Imeelezwa katika mtandao wa Zambia Reports kwamba rais huyo anakabiliwa na tatizo la kutapika.
Likikariri mtu wa karibu na wa kuaminika wa Ikului Zambia Reports wamesema kwamba Rais huyo kwa sasa haoni furaha ya kuendelea na kazi yake kutokana na kukabiliwa na maradhi mara kwa mara.
Imeelezwa kuwa Rais huyo anatapika kila anapokula kitu na kwa umri wake tatizo hilo linamfanya apoteze kiasi kikubwa cha maji mwilini mwake.
Kabvla ya kuondoka kwake inaaminika atakabidhi madaraka kwa waziri wa ulinzi Edgar Lungu na kwamba taarifa ya kukabidhi wadhifa kwa waziri huyo zimeshaelezwa.
“The President is not okay. Things are getting worse. He is leaving for South Africa tomorrow [today]. He is vomiting whatever he eats and at his age, he is losing a lot of fluids. This time around he is leaving the instruments of power with Edgar Lungu and the Secretary to the Cabinet has already been informed,” the source said.
When asked why Justice Minister Wynter Kabimba will not be the Acting President, the source said Kabimba is not liked by majority of Cabinet Ministers.
“You know Kabimba is not liked by many Cabinet Ministers, so the President came back just to come and sort out the issue of Acting President. I will keep you updated on any development,” the source said.
President Sata since coming back from Israel on Friday night been confined to his Nkwazi House, the official residence within State House, where he has spent most of the time in bed apart from the times that some selected relatives and government officials have been to visit him.
Another highly-plaved source has also revealed that the President is walking with a limp ever since he came back from the so called working holiday in Israel.
“From what we have observed, there is obviously something that is making the boss to limp but we do not know what it is,” said the source.
According to the source even the President’s voice is not as strong as it used to be. “We have noticed that he is speaking in a very low tone as if something is hindering him from speaking louder,” the source added.
The source has also revealed that President Sata does not look that strong to walk anything up to fifty meters or even stand for a long time.
“It will be a big miracle if he gets up to stand and do the swearing in ceremony of some three government officials we hear are to be sworn in,” said the source.
It’s also understood that President Sata was driven from State House on Friday night by his Press Aide George Chellah instead of the Presidential motorcade to disguise his return.
In recent days a flurry of unconfirmed reports concerning the status of the President were proven to be misleading. Unfortunately at this time, Zambia Reports was unable to obtain official acknowledgement of the report.
Meanwhile, President Sata has informed close associates he is giving up on the Presidency and in view of the confusion and divisions arising from arriving at his successor, he had instructed the party to commence preparations for a convention.
The Head of State, according to sources, want the process of his succession to have some semblance of democracy but a plan to anoint his son as PF president is in full gear.
Kabimba is expected to contest the PF top slot but President Sata has in the background told his allies within the party to rally behind Mulenga.
However, this plan to anoint Mulenga Sata may backfire has his legitimacy to contest the national presidency can be contested by Kabimba, Fred M’membe, Guy Scott, Rajan Mathani and Mutembo Nchito though an injuction.
The infamous PF cartel believes any candidate outside Kabimba is defeat in their calculated plan post Sata’s regime and would fight it tooth and nail.

Diamond Platnumz afanya makamuzi ya nguvu Kansas City, Missouri nchini Marekani

$
0
0
IMG_5447
Diamond Platnumz prezda wa wasafi akifanya makamuzi Kansas City siku ya Jumapili July 6, 2014 katika kukamulisha sherehe za uhuru wa Marekani onesha lake likihudhuriwa na mashabiki wa Afrika Mashariki wakiwemo wazawa kibao waliojitokeza kumuunga mkono.IMG_5482Diamond Platnumz akiendelea na makamuzi ndani huku akiwa amezungukwa na mashabiki wa Kansas City na wenggine wakiwa wamesafiri kutoka majimbo ya jirani.IMG_5475Mashabiki wa Diamond Platnumz wakicheza pamoja nae wakati prezda wa wasafi akiendelea kufanya makamuzi ya nguvu ndani ya Kansas City, Missouri.IMG_5445Diamond Platnumz akiendelea kufanya makamuzi ya nguvu ndani ya Kansas City MO mashabiki wengine wakipata picha mbili tatu na wengine wakiwa wanarekodi video.IMG_5463Prezda na madansa wake wakiendelea kulishambulia jukwaa Kansas City.IMG_5459Mashabiki wa Diamond wakiwa wamechanganyikiwa Prezda mwenyewe akiendelea na makamuzi ya nguvu.IMG_5448Mashabiki kama unavyoona kwenye picha wakitaka japo wamguse prezda wa wasafi kwenye show yake ya Kansas City aliyofanya siku ya Jumapili July 6, 2014 na kuhudhuriwa na mashabiki kila kona ya Missouri na Kansas na wengine wakiwa wamekuja toka majimbo mengine ya jirani.IMG_5476Mashabiki wa Diamond Platnumz wakiendelea kupagawa. Kwa picha zaidi HAPA
Viewing all 8662 articles
Browse latest View live




Latest Images