Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulucommpress@googlemail.com Website : www.ikulu.go.tz Fax: 255-22-2113425 | PRESIDENT’S OFFICE, STATE HOUSE, 1 BARACK OBAMA ROAD, 11400 DAR ES SALAAM. Tanzania. |
Dkt. Hamisi Hassan Mwinyimvua kuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha
Taarifa kamili kilichojiri kwa bondia profesheno Cheka
Bondia wa ngumi za kulipwa duniani Francis Cheka (32) amehukumiwa kifungo
cha miaka mitatu jela na kulipa fidia ya Sh. 1 milioni baada ya kutiwa hatiani kwa
kosa la kumpiga meneja wake wa baa na kwamba hukumu hiyo imemfanya mke wake aangue
kilio kizito mahakamani.
Hukumu hiyo ilitolewa leo na hakimu mkazi mwandamizi wa mahakama ya mkoa wa Morogoro Said Msuya baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka ambao haukuacha shaka yoyote katika kuthibitisha shtaka hilo.
Akisoma hukumu hiyo hakimu huyo alisema kuwa adhabu hiyo itakuwa fundisho kwa
mshtakiwa na watu wengine wanaotumia vibaya nguvu zao na kwamba mshtakiwa anatakiwa
kumlipa mlalamikaji fidia ya Sh. 1 milioni.
Hata hivyo Cheka alipewa nafasi ya kujitetea ili mahakama impe adhabu ya huruma hata hivyo aliieleza mahakama kuwa hana maelezo yoyote ya kujitetea zaidi ya kuiachia mahakama kuamua adhabu itakayompa.
Mara baada ya kutolewa kwa hukumu hiyo mke wa Cheka ambaye alishindwa
kutaja jina lake kutokana na kilio alidai kuwa mumewe ameonewa na kwamba hakustahili
kupewa adhabu hiyo.
Awali ilidaiwa mahakamani hapo na mwendesha mashtaka wa Polisi Anganile Nsiyani kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo Julai 2 mwaka 2014 katika baa ya Vijana Social Hall iliyopo Manispaa ya Morogoro.
Mwendesha mashtaka huyo alidai kuwa bila halali na akijua kufanya hivyo ni kosa Cheka alimshambulia meneja wake wa baa aliyefahamika kwa jina la Bahati Kibanda kwa kumpiga ngumi usoni na tumboni na hivyo kumsababishia maumivu makali.
Alipofikishwa mahamani hapo kwa mara ya kwanza Chekaalikana shtaka hilo na hivyo upande wa mashtaka uliamua kupeleka mashahidi wane kati ya saba ambao waliithibitisha mahakamani hapo bila ya shaka kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo na hivyo mahakama kumtia hatiani.
Mwisho….
KIPA BORA WANAWAKE AZAWADIWA 500,000/-
Kipa bora wa michuano ya Kombe la Taifa la Wanawake, Belina Julius wa
Temeke amezawadiwa sh. 500,000 na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo, Dk Fenella Mukangara.
Dk Mukangara alitoa zawadi hiyo baada ya mechi ya fainali ya michuano
iliyomalizika jana kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi jijini Dar
es Salaam. Dk Mukangara alikuwa mgeni rasmi kwenye fainali hiyo.
Temeke ndiyo walioibuka mabingwa wa michuano hiyo iliyofanyika kwa mara ya
kwanza nchini baada ya kuilaza Pwani bao 1-0 katika fainali iliyoonyeshwa
moja kwa moja (live) na televisheni ya Azam.
Ilala ilifanikiwa kutwaa baada ya kuichapa Kigoma mabao 3-0. Bingwa amepata
sh. milioni tatu, makamu bingwa sh. milioni mbili wakati mshindi wa tatu
ameondoka na sh. milioni moja katika michuano hiyo iliyodhaminiwa na
kampuni ya Proin.
TFF YATOA RAMBIRAMBI MSIBA WA KATIBU IRFA
**
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko
taarifa ya msiba wa Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa
Iringa (IRFA), John Ambwene Mwakalobo uliotokea jana (Februari 1 mwaka huu)
mkoani Iringa baada ya kuanguka akiwa nyumbani kwake.
Msiba huo ni pigo kwa wadau wa mpira wa mpira wa miguu kwani wakati wa uhai
wake, Mwakalobo alitoa mchango mkubwa akiwa kiongozi. Mwaka 2011
alichaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa IRFA, kabla ya 2012 kushinda nafasi
ya Katibu Msaidizi.
Alizaliwa Februari 4, 1954 na kupata elimu ya sekondari katika shule ya
Azania, Dar es Salaam na baadaye mafunzo ya ualimu kwenye Chuo cha Ualimu
Mpwapwa mkoani Dodoma. Alianzia kazi ya ualimu Newala mkoani Mtwara kabla
ya kuhamia mkoani Iringa mwaka 1981. Alistaafu mwaka 2013.
TFF inatoa salamu za rambirambi kwa familia ya marehemu, na Chama cha Mpira
wa Miguu Mkoa wa Iringa (IRFA) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu
katika kipindi hiki kigumu kwa msiba huo.
Marehemu anatarajiwa kuzikwa kesho (Februari 3 mwaka huu) kwao Kyela mkoani
Mbeya. Ameacha mke, watoto wanne na mjukuu mmoja. Bwana alitoa, Bwana
ametwaa. Jina lake lihimidiwe.
*IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)*
TFF MBIONI KUPATA MDHAMINI FDL
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) liko mbioni kupata mdhamini wa
Ligi Daraja la Kwanza (FDL). Tunatarajia mdhamini huyo atakuwa tayari kwa
ajili ya msimu wa 2015/2016.
Ligi Daraja la Kwanza inashirikisha timu 24 zinazocheza katika makundi
mawili ya timu 12 kila moja kwa mtindo wa nyumbani na ugenini.
Timu zinazocheza FDL msimu huu ni African Lyon (Dar es Salaam), African
Sports (Tanga), Ashanti United (Dar es Salaam), Burkina Faso (Morogoro),
Friends Rangers (Dar es Salaam), Geita Gold (Geita), Green Warriors (Dar es
Salaam), JKT Kanembwa (Kigoma), JKT Mlale (Ruvuma) na JKT Oljoro (Arusha).
Nyingine ni Kimondo (Mbeya), Kinondoni Municipal Council (Dar es Salaam),
Kurugenzi (Iringa), Lipuli (Iringa), Majimaji (Ruvuma), Mwadui (Shinyanga),
Panone FC (Kilimanjaro), Polisi Dar es Salaam, Polisi Dodoma, Polisi Mara,
Polisi Tabora, Rhino Rangers (Tabora), Toto Africans (Mwanza), na Villa
Squad (Dar es Salaam).
MECHI ZA MWISHO FDL SASA FEB 8 NA 10
Mechi za raundi mbili za mwisho za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kwa makundi
yote mawili zimerudishwa nyuma kutokana na maombi ya klabu hizo kupungaza
gharama za kuendelea kuziweka kambini timu zao.
Hivyo, Februari 8 mwaka huu kundi A litacheza mechi zake za raundi ya 21
wakati zile za raundi 22 ambayo ndiyo ya mwisho zitafanyika Februari 13
mwaka huu. Mechi za Februari 8 ni KMC vs African Lyon, Kurugenzi vs African
Sports, Majimaji vs JKT Mlale, Kimondo vs Friends Rangers, Ashanti United
vs Villa Squad, Polisi Dar vs Lipuli.
Februari 13 mwaka huu ni African Lyon vs Polisi Dar, Kurugenzi vs Lipuli,
Kimondo vs Majimaji, JKT Mlale vs Ashanti United, Friends Rangers vs
African Sports, na Villa Squad vs KMC.
Kwa upande wa kundi B wataanza mechi za raundi 22 Februari 10 mwaka huu ili
kupisha mechi za viporo za Polisi Mara zinazomalizika Februari 5 mwaka huu.
Hivyo, Februari 10 mwaka huu itakuwa ni Burkina Faso vs JKT Kanembwa,
Mwadui vs Polisi Tabora, Polisi Dodoma vs Green Warriors, Rhino Rangers vs
JKT Oljoro, Panone vs Polisi Mara, Geita Gold vs Toto Africans.
Raundi ya 22 itachezwa Februari 15 mwaka huu kwa mechi kati ya JKT Kanembwa
vs Green Warriors, Mwadui vs Burkina Faso, Polisi Tabora vs JKT Oljoro,
Polisi Dodoma vs Panone, Toto Africans vs Rhino Rangers, na Geita Gold vs
Polisi Mara.
Waainjilisti wa Kikristo wapinga mahakama ya kadhi ndani ya mfumo rasmi wa utawala
WAZIRI MKUU AVUTIWA NA SHAMBA LA KAHAWA SONGEA
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema amevutiwa sana na kazi iliyofanywa katika muda mfupi kwenye shamba la kahawa la Aviv lililoko kwenye kijiji cha Lipokela, wilaya ya Songea Vijijini mkoani Ruvuma.
Amesema katika kipindi cha mwaka mmoja na miezi saba, eneo kubwa la shamba limepandwa miche ya kahawa na mingine imezaa na imeshavunwa ikilinganishwa na wakati alipofika shambani hapo Julai 2013 na kutembelea tu kitalu cha miche ya zao hilo.
Ametoa kauli hiyo jana jioni (Jumatatu, Februari 2, 2015) wakati akizungumza na wafanyakazi na menejimenti ya shamba la Aviv baada ya kulitembelea na kukagua miundombuinu ya umwagiliaji wa matone ya maji kwenye shamba hilo.
“Mkuu wa shamba hili, Bw. Medu amenieleza kwamba mpaka sasa, wameshavuna kahawa mara moja na wanatarajia kuvuna tena hivi karibuni; lakini ili waweze kuanza kupata faida ni lazima wavune mara nne.”
“Kilimo kinataka uvumilivu na kinataka uwekezaji mkubwa... ni lazima kiwepo; hata kwa wakulima wadogo ni lazima kiwepo licha ya ugumu wake. Sasa ukisema kilimo ni kigumu na ukaacha kulima wakati una mke na watoto, je hao watakula wapi?”, alihoji.
Aliwasifu wamiliki wa shamba hilo kwa kuchagua kulima zao la kahawa kwani lina walaji kila mahali ulimwenguni kote. “Wameamua kulima kahawa aina ya Arabicaambayo inakubalika duniani. Uhitaji wa kahawa hii upo kila mahali kwa sababu wanywaji wapo,” alisema.
Waziri Mkuu alisema pamoja na mafanikio hayo, shamba la Aviv linakabiliwa na changamoto ya nishati kwani linahitaji megawati 2.5 ili liweze kuendesha mitambo yake ambayo kwa sasa inatumia mafuta yanayoligharimu fedha nyingi.
Aliwataka wamiliki wa shamba hilo waendelee kuwa wavumilivu wakati Serikali ikiendelea kutafuta ufumbuzi wa suala hilo.
Mapema, akisoma risala ya kampuni ya Aviv, Mkuu wa shamba hilo ambaye pia anasimamia uzalishaji wa zao la kahawa Afrika Mashariki, Bw. Medu Medappa alisema hadi sasa wamekwishalima hekta 1,060 na zote zimekwishawekewa miundombinu ya umwagiliaji wa matone na kati ya hizo, hekta 810 zimekwishapandwa miche ya kahawa.
“Shamba letu lina ukubwa wa hekta 2,000 na hadi sasa tumeshalima hekta 1,060 na zilizobakia ni kwa ajili ya kutunza mazingira na uoto wa asili kwenye vilima vinavyotuzunguka,” alisema.
Alisema hadi sasa wamekwishaajiri wafanyakazi 1,500 kwenye shamba hilo na kutoa mafunzo kwa wakulima wanaoishi vijiji vya jirani. “Pia tumewapatia miche ya bure kaya 673 na kutokana na mafunzo tunayowapa, wanavijiji wameweza kulima kahawa inayoendana na viwango vya kimataifa vya uzalishaji kahawa ambavyo ni miezi 22,” alisema.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Bw. Said Mwambungu akijibu moja ya hoja kwenye risala ya Bw. Medappa iliyohusu eneo la hekta tisa kuchukuliwa na Wakala wa Ujenzi wa Barabara (TANROADS), alisema eneo hilo ni muhimu kwa ujenzi wa barabara za mkoa huo kama ambavyo shamba hilo ni muhimu kwa mkoa huo.
“Lile eneo limetengwa na TANROADS kwa ajili ya kutengeneza kokoto za ujenzi wa barabara. Barabara za lami tunazitaka. Tunahitaji kazi hii iendelee la sivyo barabara zetu zitakufa,” alisema.
Alisema watu wa TANROADS wakimaliza kazi yao, lile eneo litabaki tupu na mwekezaji huyo anaweza kulitumia kadri atakavyoona inafaa kwa sababu liko ndani ya eneo lake.
(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, FEBRUARI 3, 2015.
DKT. NCHIMBI ASEMA CCM HAINA TATIZO LA KIMUUNDO WALA MFUMO
Kigoma yakumbwa na kipindipindu, watano wafariki
WATU watano wamekufa na wengine zaidi ya 170 wamelazwa kufuatia mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu ulioukumba mkoa Kigoma.
Akizungumza mjini Kigoma leo Mganga Mkuu wa mkoa kigoma,Leonald Subi amesema kuwa Manispaa ya Kigoma Ujiji imeathirika kwa kiasi kikubwa na ugonjwa huo na kwamba tayari hatua mbalimbali zimechukuliwa kukabiliana na hali hiyo.
Subi alisema kuwa tangu mwezi Januari mwaka huu ugonjwa huo ulioanza kuripotiwa kwenye wilaya ya Kasulu na manispaa ya Kigoma Ujiji watu 175 walikuwa wamekumbwa na ugonjwa huo katika manispaa ya Kigoma Ujiji huku wilaya ya Kasulu ikiwa na wagonjwa wanane.
Alisema kuwa kwa manispaa ya kigoma Ujiji eneo lililoathiriwa ni kata ya kibirizi ambako sehemu kubwa ya wagonjwa waliougua na kufariki walitoka huko na kwamba tayari kambi ya wagonjwa wa kipindu pindu imefunguliwa kwenye kituo cha afya cha Gungu Manispaa ya Kigoma Ujiji.
Washauriwa kuacha kuosha uke kwa mvuke
Ukiangalia video hiyo unaweza kabisa kusema ni vyema na wewe (mke) ukapigwe na stimu mambo yaende safi, lakini hapa pana maneno yasome.
WATAALAMU wameingiza maneneo katika kampeni kubwa inayoendeshwa na Gwyneth Paltrow ya kusafisha uke kwa mvuke.
Wataalamu wamesema tabia hiyo inayopigiwa debe na muigizaji huyo si nzuri na kuna hatari ya kuharibu utaratibu wa kawaida wa uke.
Hayo yameandikwa na jarida moja la Marekani.
Katika makala yake imesema kwamba pamoja na Gwyneth Paltrow kupigia debe shughuli hiyo na kushawishi watu wanaofika Mji wa Los Angeles kuhakikisha wanafika katika kliniki yake na kufanyiwa au kupewa maelekezo ya namna ya kusafisha uke na mvuke.
Muigizaji huyo anasema kwamba tiba yenyewe ni nyepesi tu kwani unachofanya unakaa kwenye kiti na unaachia mchanganyiko uliomo kwenye mvuke kufanyakazi ya kutakasa sehemu zako za kizazi.
Huduma hiyo ina gharimu dola 50 lakini madaktari waliozungumza na NewsBeat wanasema hawana uhakika na usalama wala faida ya tiba hiyo.
Tikkun Spa wanasema kwamba huduma hiyo husaidia kutibu hali mbalimbali ikiwamo ya kuhami tumbo la uzazi dhidi ya kansa na majipu.
Pamoja na maelezo hayo, wanaohusika natiba hiyo wanakiri kwamba haijatathminiwa wala kukubaliwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa ya Marekani.
Pamoja na ukweli huo, madaktari wanasema kwamba uke umetengenezwa kwa namna ya kwamba unajitunza wenyewe kutokana na majimaji yeye dawa yanayotoka mwilini.
Wataalamu hao wamesema kwamba usafishaji wa uke kwa namna hiyo si lazima utafanya uwe msafi na salama.
"Utoko katika uke si lazima uwe ni dalili mbaya," anasema Dk Suzy Elneil, Mtaalamu wa ushauri wa masuala ya uke wa Hospitali ya Chuo Kikuu cha London.
"Kuna kauli zinazoamini kwamba utoko huo unaambatana na magonjwa ya zinaa, hii si kweli." alisema na kuongeza kuwa mabadiliko katika utoko uwingi au uchache wake unaweza kuwa ni shida ya homoni ambayo inaunganishwa kwenye mzunguko wa hedhi wa mwanamke.
Aidha matumizi ya mvuke, sabuni zinazonukia, jeli, dawa za kuua wadudu zinaweza kabisa kubadilisha afya ya uke na mizania ya pH.
Madaktari wanasema ni vyema wanawake wakatumia sabuni zisizo na pafyumu kusafishia sehemu ya nje ya na ndani ni kazi ya asili kusafisha, uke wenyewe unajisafisha kwa kutumia kemikali mbalimbali zilizopo.
"Siwezi kufikiria kwamba usafishaji wa uke kwa kutumia mvuke (kuflashi kwa maneno mengine) kunasaidia. Kwa kufanya hivyo utaondoa na bakteria muhimu wanahitajika kwa ajili ya kusafisha na kuuliza uke," anasema Professora Ronnie Lamont wa Royal College of Obstetricians and Gynaecologists.
Wataalamu wamesema matumizi ya mvuke kama ilivyo katika matumizi mengine inaweza kuleta madhara katika uke.
Filamu kwenda 'Buku Jero' ni kizunguzungu cha ukweli
Kampuni hii pamoja na kusambaza sinema , bali pia ilianza kuwa executive producer ikitoa fedha kwa skripti mbalimbali na hivyo kimantiki kumiliki sinema hizo.
OLOLOSOKWAN WAPIGWA MSASA KUKITUMIA VYEMA KIJIJI CHA DIJITALI

Afisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) Bw. Al Amin Yusuph akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues (aliyeipa mgongo kamera) wakati wa ukaguzi wa mwisho wa eneo la mradi wa kijiji cha digitali wa Samsung unaoendeshwa na UNESCO lilitolewa na serikali ya kijiji. Katikati ni Mwenyekiti wa kijiji cha Ololosokwan wilaya ya Ngorongoro, Kerry Dukunyi .(Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog)
Na Mwandishi wetu, Ngorongoro
SHIRIKA la Elimu ,sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa, UNESCO, limeanza maandalizi ya kuumilikisha mradi wa kijiji cha digitali cha Ololosokwan kwa wananchi wa kijiji hicho kwa kuendesha warsha ya siku mbili ya kutambua vipaumbele vya wananchi vitakavyoingizwa katika mradi huo.
Vipaumbele hivyo ni katika elimu, afya na uchumi.
Warsha hiyo ilishikirikisha wanakijiji wa Ololosokwan na vijiji vingine vinavyozunguka kijiji hicho,viongozi wa halmashauri, viongozi wa kimila, viongozi wa vijiji na wataalamu mbalimbali wa sekta ya afya, elimu na uchumi.
Katika majadiliano yao wananchi walitambua changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo ambazo zina uhusiano wa moja kwa moja na mazingira na mfumo wa utamaduni walionao wakazi wa eneo hilo.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akikagua eneo la mradi wa kijiji cha kidigitali Ololosokwani wilayani Ngorongro. Kushoto ni Mwenyekiti wa kijiji cha Ololosokwan, Kerry Dukunyi na Mratibu wa miradi wa Taasisi ya Irkiramat, Salanga Mako.
Wakazi hao ambao ni wafugaji wenye kuheshimu mila na utamaduni wa kimasai na mfumo wa maisha wamesema kwamba lugha inayotumika katika kufundishia ni tatizo na ingawa wana shule mbili za msingi na sekondari lugha ya Kiswahili ni tatizo na wakifika sekondari lugha ya kiingereza nayo inakuwa tatizo.
Aidha walisema kutokana na wazazi kutokuwa na elimu hawaoni sababu ya kuwafanya watoto wao wenye maarifa makubwa kwenda shule na badala yake hao wanaoelewa vitu hupelekwa kuchunga au wale wenye umri mdogo wa kike huolewa.
Warsha hiyo pia ilibainisha tatizo la afya ya wanawake na watoto, ndoa za utotoni na magonjwa ya zinaa ya kuambukiza.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akiteta jambo na ujumbe wake aliombatana nao kwenye kijiji cha Ololosokwan kwa ajili ya kuwapiga msasa wananchi wa kijiji hicho ikiwa ni maadalizi ya kupokea mradi wa kijiji cha kidigitali hivi karibuni.
Kijiji hicho cha digitali ambacho ni nadharia ya Samsung katika kurejesha faida kwa umma kitakuwa na huduma mbalimbali ambazo zikiunganishwa na haja ya wananchi zitasaidia kubadili maisha ya wamasai na kuondokana na utegemezi wa mifugo pekee na kutambua thamani yao katika rasilimali zilizopo katika maeneo yao.
Warsha hiyo ambayo imesimiwa na wataalamu kutoka UNESCO imelenga kuwafungua macho na kuwashirikisha wananchi kuhusu mradi huo mkubwa wa aina yake nchini na duniani.
Kijiji cha dijitali nchini Tanzania ni cha nne cha kwanza kikiwa nchini Afrika Kusini, kingine Gabon na Ethiopia.
Baadhi ya wanakijiji wa Ololosokwan na vijiji vingine vinavyozunguka kijiji hicho,viongozi wa halmashauri, viongozi wa kimila, viongozi wa vijiji na wataalamu mbalimbali wa sekta ya afya, elimu na uchumi wakimsikiliza Mkurugenzi mkazi wa UNESCO, Zulmira Rodrigues (hayupo pichani).
Kijiji hicho ili kiwe endelevu wananchi wanaohusika wanatakiwa kuelewa mradi huo kuweka vipaumbele vyao na kuangalia jinsi ya kutumia mradi huo katika kukabili changamoto zinazowakabili kwa sasa.
Katika majadiliano kwenye ngazi za elimu wananchi walielezea haja ya kushawishi wamasai kuanza kujifunza Kiswahili na Kiingereza ili kuweza kufuatilia kwa karibu masomo na pia kuwepo kwa sheria ndogo ili kuzuia utoro wa wanafunzi kwa ajili ya kwenda kuchunga mifugo na pia kuolewa mapema kwa mabinti.
Mathias Herman, mratibu wa program za Afya , UNESCO, alisema kwamba pamoja na kwamba kijiji hicho kitakuwa na zahanati na huduma za mawasiliano ya tiba (telemedicine) hamasa kubwa inatakiwa kutolewa ili wananchi waweze kutumia huduma hizo kwani kwa sasa wamejikita zaidi huduma za waganga wa jadi.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akiendesha mjadala kwa wanakijiji wa Ololosokwan na vijiji vingine vinavyozunguka kijiji hicho,viongozi wa halmashauri, viongozi wa kimila, viongozi wa vijiji na wataalamu mbalimbali wa sekta ya afya, elimu na uchumi ikiwa ni maandalizi ya kuupokea mradi wa kijiji cha kidigitali Ololosokwani wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.
Alisema katika warsha kulielezwa kuwa kukosekana kwa madaktari katika zahanati zilizopo kijijini hapo kumefanya watu wengi kuendelea kuamini waganga wa jadi na kujifungulia huko hali ambayo imezaa kuwapo kwa idadi kubwa ya wanawake wanaokufa wakati wa uzazi na pia watoto wasiopata chanjo.
“Wakifika hakuna madaktari hawawezi kuamini huduma hii wakati kuna waganga wa kienyeji na wakunga wa kienyeji” alisema Mathias na kuongeza kuwa katika warsha ilihimizwa kwamba watu watambue tatizo lililopo la kiafya linalosababishwa na mfumo wa mazingira na maisha ya wafugaji na kuhakikisha kwamba huduma zinazoletwa zinatumiwa vyema.
Aidha alisema kuwapo kwa kiwango kikubwa cha maambukizi ya magonjwa ya zinaa, ndoa za utotoni na mimba katika umri mdogo ni sehemu ya matatizo ambayo yanaaminika kwamba yanaweza kutanzuliwa kwa kutolewa elimu na kushawishi wakubwa wa mila kutambua nafasi zao na elimu ya kisasa katika kushughulikia changamoto za kiafya.
Afisa mipango ya Elimu wa Shirika la UNESCO, Bi. Jennifer Kotta (kulia) akiwa kwenye majadiliano na baadhi ya wanakijiji wa Ololosokwan kuhusiana na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya elimu na nini kifanyike kuboresha sekta ya elimu kwa ujumla katika kijiji hicho na kuishirikisha halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro katika maandalizi ya kupokea mradi wa kijiji cha kidigitali.
“mila na heshima kwa wakubwa wa mila kumefanya wamasai kutegemea tiba za asili na mfumo wa asili wa kuendesha maisha bila kujua athari kwao ziwe hasi au chanya” alisema Mathias kauli iliyoungwa mkono na Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO, Zulmira Rodrigues ambaye alisema kunahitajika sana ushirikiano wa jamii, viongozi, wazazi kuhakikisha kwamba kijiji kinafanikiwa na kuwa cha kupigiwa mfano.
Kijiji cha Ololosokwan kilichopo Loliondo, wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha kikiwa na watu 9000 kupitia mradi huo kitapewa pia mbinu za kuimarisha soko la utalii, kulitambua na kulitumia kwa manufaa yao na pia elimu ya ubunifu ambayo itawafanya wanawake wanaotengeneza urembo mbalimbali kuweza kumudu soko la utalii na la kawaida.
Afisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) Bw. Al Amin Yusuph akiendesha mjadala na baadhi ya wanakijiji wa Ololosokwan kuhusiana mradi wa kijiji cha kidigitali na kuuboresha ili kutatua matatizo ya wananchi pamoja na kuwapata taarifa za maendeleo kupitia redio jamii ya Loliondo FM inayofadhiliwa na UNESCO ikiwa ni katika maandalizi ya kuupokea mradi huo wa kijiji hicho unaotarajiwa kuwasili hivi karibuni kijijini hapo.
Aidha mradi huo utafikisha umeme na elimu kwa njia ya Tehama huku, elimu hiyo ya Tehama ikikusudiwa kutumika kutoa elimu ya darasani kwa wanafunzi ambao wapo machungani.
Mfumo wa wamasai ambao umejengwa katika utamaduni na kuthamini mifugo unatakiwa kubadilishwa kwa wazazi kupewa elimu ya kuwawezesha kutambua umuhimu wa elimu kwa watoto wao.
Afisa Mradi wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias akiongoza mjadala wa nini kifanyike katika kuboresha sekta ya afya na changamoto zinazowakabili wanakijiji wa Ololosokwan kwa ajili ya maandalizi ya kuupokea mradi wa kijiji cha Kidigitali unaoendeshwa na UNESCO kwa kushirikiana na kampuni ya Ki-elektroniki ya Samsung unaotarajiwa kuwasili mapema mwezi februari kijijini hapo. Wa pili kushoto ni Mratibu wa Taifa wa tiba asilia na mbadala katika Idara ya Tiba Wizara ya Afya na ustawi wa jamii. Dkt Liggy Vumilia.
Afisa mipango ya Elimu wa Shirika la UNESCO, Bi. Jennifer Kotta akiwasilisha kazi ya kikundi chake baada ya kujadiliana na wanakijiji wa Ololosokwan katika kuboresha sekta ya elimu ikiwa ni maandali ya kupokea mradi wa kijiji cha kidigitali kinachotarajiwa kuwasili hivi karibuni kijijini hapo.
Mmoja wa washiriki wa kikundi kilichokuwa kikijadili masuala ya utamaduni na utalii akiandika changamato mbalimbali zinazowakabili wakinamama wakimasai wanaofanya biashara za urembo wa kimasai kwa watalii wanaotembelea hifadhi ya Ngorongoro.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akishiriki kwenye mjadala na wanakijiji wa kijiji cha Ololosokwan katika maandalizi ya kupokea mradi wa kijiji cha kidigitali unaotarajiwa kuwasili mapema mwezi februari kijiji hapo.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akisaini mkataba wa kukabidhiwa ardhi iliyotolewa na serikali ya kijiji kwa ajili ya mradi wa kijiji cha kidigitali huku tukio hilo likishishudiwa na uongozi wa juu wa serikali ya kijiji, wataalam kutoka UNESCO na halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro pamoja na wanakijiji.
WAMILIKI WA VIWANDA WATAKIWA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADADISI WA SENSA YA VIWANDA.
![]() |
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Maria Bilia akiwa katika picha ya pamoja na menejimenti ya NBS na wadadisi wa Sensa ya Viwanda |
Source: Aron Msigwa – MAELEZO
ELEPHANT LIVE COMES WITH THAIS DIARRA IN CONCERTS
BREAKING NEWS! ASKARI AUAWA AKIKAMATA MSHTAKIWA
RAIS KIKWETE AONGOZA SHEREHE ZA SIKU YA SHERIA NCHINI LEO JIJINI DAR ES SALAAM
MULTICHOICE YAZINDUA KING’AMUZI KIPYA CHA DStv HD

Meneja Uhusiano wa MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi (Katikati) akifafanua jambo kwenye mkutano na wanahabari (hawapo pichani), wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa king'amuziki kipya cha DStv HD leo jijini Dar. Kulia ni kwake ni Meneja uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo na kushoto ni Meneja Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu.(Picha na Zainul Mzige wa modewjiblog)
Na Andrew Chale
KAMPUNI ya MultiChoice Tanzania wasambazaji wa ving’amuzi vya DStv, leo imezindua king’amuzi kipya cha DStv HD ambacho kitaanza kutumika kwa mara ya kwanza hapa Nchini.
Akizungumza na wandishi wa habari mapema leo jijini Dar es Salaam, Meneja Uendeshaji wa MultiChoice Tanzania, Ronald Shelukindo, akielezea umuhimu wa huduma hizo alisema king’amuzi hicho kina ubora wa hali ya juu ikiwemo kuonyesha picha zenye ubora mzuri zaidi.
Pia alieleza kuwa, DStv HD mteja atapata kuona picha zenye mvuto zaidi pamoja na kiwango cha juu cha sauti Dolby Digital 5.1.
“Wateja wa DStv watafurahia ving’amuzi hivi kwa ubora wa hali ya juu hivyo ni wakati wa kuchangamkia ofa kwani ndio mara ya kwanza kuingia kwa Tanzania” alisema Ronald Shelukindo.
Meneja uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo akielezea ubora wa king'amuzi hicho cha DStv HD wakati wa mkutano huo na waandishi wa habari leo jijini Dar.
Ronald Shelukindo akielezea kwa kina, alisema DStv HD, mteja anaweza kufurahia vipindi mbalimbali ikiwemo mifumo na mipangilio ya kila vipindi kwa kupendekeza atazame kipi gani, muda gani na wakati gani?.
King’amuzi cha “DStv HD, mteja anaweza kujipangia atazame kipindi gani ama kwa wakati autakao yeye, ambapo anachoweza ni kuseti hicho kipindi akipendacho na kisha anaweza kukiangalia kwa wakati wake, hata kama muda umepita kwa wakati huo kinarushwa kwenye chaneli husika” alifafanua Ronald Shelukindo.
Kwa upande wake, Meneja Masoko wa MultiChoice Tanzania, Furaha Samalu aliwahimiza watanzania kuchangamkia vinga’muzi hivyo vya DStv HD, ambavyo kwa sasa vipo karibu maduka yote ya Mawakala wa DStv, kwa bei rahisi kabisa vikiwa vinapatikana kwa sh 99,000/ kwa mteja mpya huku kwa wateja walio na ving’amuzi vya zamani vya DStv watakaotaka kubadilishiwa, watalipia sh 39,000/ tu.
Meneja uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo akionesha king'amuzi kipya cha DStv HD kwa waandishi wa habari (hawapo pichani).
“Ofa hii ni kwa ajili ya kipindi hiki cha fainali za AFCON, hadi hapo michuano hii itakapofikia tamati ambapo bei itabadilika kutoka hizi za sasa, hivyo ni wakati wa kuchangamkia ofa hii ya kipekee na kwa mara ya kwanza, kupata kitu cha ubora wa hali ya juu na kwa bei rahisi.” Alisema Furaha Samalu.
Kwa upande wake, Afisa Uhusiano wa MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi alieleza kuwa, siku zote MultiChoice itaendelea kuwa mstari wa mbele kwa kutoa huduma zilizo bora na za kisasa katika ulimwengu huu wa digitali ambapo bidhaa hizo za DStv zimeendelea kuwa bora kila siku.
“Huduma za DStv siku zote zimekuwa bora ikiwemo kutoa huduma zisizoleta usumbufu. Ving’amuzi vyetu daima vinaonyesha ubora wa hali ya juu na hutoweza kusumbuliwa na ukatikaji wa picha ama mikwaruzo... Hivyo ni wakati sasa wa kuchangamkia ofa hizi.” Alibainisha Barbara Kambogi.
Meneja Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu akifafanua bei za king'amuzi hicho kipya ambapo kwa wateja wapya watajipatia kwa ofa ya Tsh. 99,000/ kuanzia leo hadi siku Jumapili kilele cha fainali za michuano ya AFCON huku ambao ni wateja tayari wanabadilishiwa kwa gharama ya Tshs. 39,000/ ambayo pia ni ofa. Ving'amuzi hivyo vipya vya DStv HD vinapatikana kupitia mawakala wote wa DStv Tanzania nzima.
Katika hatua nyingine, DStv wamezindua huduma mpya kwa wateja wao waliounganishwa na ving’amuzi hivyo vya DStv kuweza kuendelea kufurahia huduma hiyo kupitia simu zao za viganjani zenye uwezo wa ‘Android’, Kompyuta mpakato (Laptop), Tablet, na vifaa vingine vyenye uwezo wa kupokea usajili wa ‘App’.
Akielezea, juu ya huduma hiyo, Ronald Shelukindo, alibainisha kuwa, kinachotakiwa ni kwa mteja wa DStv, kwenda kwenye simu yake au Laptop, ama Tablet na kisha kujisajili kupitia ‘App’ kwa kujisajili kwa kuandika ‘DStv Now’.
Aidha, Ronald Shelukindo alisisitiza kuwa, huduma hiyo ya DStv Now ni kwa wateja waliouganishwa na ving’amuzi hivyo tu ambapo wataifurahia huduma hiyo kwa kuendelea kuangalia chaneli zaidi ya 12 za DStv, ikiwemo ya Super Sport 3, za filamu, na nyinginezo mbalimbali.
Pia kwa maelezo zaidi wateja wanaweza kutembelea tovuti ya DStv.com
Meneja uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo akionesha huduma mpya ya DStv Now ambayo mteja ataweza kuangalia vipindi vya DStv kupitia simu yake ya kiganjani, kompyuta mpakato (Laptop) pamoja na Tablet. Huduma hii ni kwa wateja ambao wameunganishwa na ving'amuzi vya DStv kupitia akaunti zao.
Meneja Uhusiano wa MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi (katikati), Meneja uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo (kulia) na Meneja Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu (kushoto) wakiangalia promo ya namna ya kujiunga na huduma ya DStv Now "application" inayopatikana katika simu zote za Android pamoja na kompyuta mpakato (Laptop) unajiunga kwa kutembelea www.dstv.com
Baadhi ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakifuatilia uzinduzi huo uliofanyika jijini Dar leo.
Meneja uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo (katikati) na Meneja Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu (kulia) na Meneja Uhusiano wa MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi (kushoto) wakipozi na king'amuzi kipya cha DStv HD.
Kamanda Misime aeleza kilichomuua askari wake
![]() |
Pc swai enzi za uhai wake |
Msako bado unaendelea ili kuweza kumtia nguvuni mtuhumiwa huyu aliyesababisha kifo cha askari wetu wakati alipojitolea maisha ya ili kumwokoa huyo mtoto mdogo.
Kamanda Misime amesema Malya mwenye umri wa miaka 29 ni na kwa kabila mchaga ni maji ya kunde, mwembamba, siyo mrefu sana saizi ya kati na alikuwa amevaa suruali rangi ya blue iliyopauka na T-Shirt rangi ya dark blue na kofia nyeupe yenye alama nyekundu .