Quantcast
Channel: Lukwangule Entertainment
Viewing all 9274 articles
Browse latest View live

AMIRI JESHI MKUU JAKAYA KIKWETE ATEMBELEA VIKOSI VYA JWTZ VYA KOMANDO NA UHANDISI MEDANI

$
0
0

Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili kwenye Kikosi cha Komando kuanza ziara yake ya kujionea hali na utimamu wa vikosi vya JWTZ Mkoani Morogoro.



Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipewa maelezo kwa kutumia mchoro kuonesha mzunguko mzima wa maeneo atakayotembelea katika kikosi cha Komando.


Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia kupitia kilengeo maalum kinachotumiwa kwenye silaha na makomando kulengea shabaha.

Makomando wakimuonesha Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (hayuko pichani) mapigano bila silaha wakati wa ziara yake.


Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akivuka juu ya daraja jipya la medani lililojengwa kumuonesha uwezo wa Wahandisi Medani wa JWTZ kuendelea kusaidia usafirishaji wa zana na vifaa hata pale madaraja ya kudumu yanapoharibiwa kwa namna yoyote ile.

(Na Luteni Kanali Juma Nkangaa Sipe, Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Ulinzi na JKT. Email: jnisipe@gmail.com. Simu: +255 756448787, +255 784370500 na +255 655 878744)


·         >ARIDHISHWA NA UTIMAMU WA VIKOSI HIVYO KIMAFUNZO NA ZANA
·         >AAHIDI TATIZO LA MAJI KUPATIWA UFUMBUZI NDANI YA MWAKA 2014
·     >KIKOSI CHA UHANDISI WA MEDANI CHAAHIDIWA VIFAA ZAIDI ILI KUPAMBANA NA MAJANGA NCHINI
·        > AAGIZA JWTZ KUBUNI MIKAKATI YA KUONDOKANA NA MAKAZI YA MUDA

ukumbi wa mikutano wa bunge kwa jicho la Michuzi

$
0
0
Muonekano wa ukumbi wa bunge ambako Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba mjini
Dodoma ambamo Wajumbe wanakutana kujadili rasimu ya kanuni za Bunge Maalum
za mwaka 2014 leo

Picha na Muhidin Issa Michuzi-

hali ya hewa watangaza matata ya mvua

*AFANDE SELE AACHIA MWENDO KASI-'chini ya Flexible Music'*

$
0
0






Moja kati ya studio ambayo inafanya vizuri katika utayarishaji wa muziki
jijini dar es salaam sinza lego Flexible music imekuja tena na Mfalme wa
Rhymes Afande Sele na ngoma yake mpya inayoitwa Mwendo kasi aliyoifanya
katika studio hizo.

Mwendo kasi ni ngoma ambayo inaelezea ajali mbali mbali zinazotokea
barabarani ambazo zinasababishwa na uzembe wa madereva na kusababisha vifo
vya wananchi, akiwa amewashrikisha wasanii kutoka mkoani Morogoro Dyna
Nyange na Ballet.

Pia wimbo huo ambao umetengenezwa na mtayarishaji kutoka Flexible Music
anayeitwa Mbatizaji akiwa ameutengeneza kwa kiwango cha hali ya juu
kutokana na vyombo na ubora wa studio, hata hivyo katika wimbo huo ambao
umefafanua mambo mengi yatokeayo barabarani.

Kwa mashabiki wa Afande Sele mkae tayari kwa kile kitu ambacho
amekizungumza katika wimbo huo maana amezungumza mengi  kama unavyojua
Mfalme wa Rhymes huwa akitoa kitu hakosei kwa mashabiki wake.

Katika wimbo huo amewazungumzia kwa wale madereva ambao wanakunywa pombe
kisha wanaingia barabarani kumata uskani na kuendesha gari kwa mwendo wa
kasi na kusababisha ajali pia ameongea kuhusu abiria ambao wanakaa kimya
wakati dereva akiwa anaendesha gari kwa kasi.

Na Pia kwa madereva ambao wanaongea na simu huku wanaendesha magari, pia ku
overtake katika kona kali maana nao wanaweza kusababisha ajali na kupoteza
uhai wa binadamu maana uhai hauji mara mbili.

Airtel yazindua huduma ya Breaking news kupitia simu

$
0
0

Airtel imezindua huduma mpya ya utaoaji wa taarifa za hapo kwa papo .
Huduma hiyo inayojulikana kama Airtel Mwananchi Breaking news itahusisha utoaji wa habari kupitia wateja wa simu za mkononi wanaotumia mtandao wa Airtel kwa kushirikiana na Kampuni ya Mwananchi Communications inayochapisha magazeti ya Mwananchi.
 Akizungumza wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa huduma hiyo Mkurugenzi Mwendeshaji wa Mwananchi Francis Nanai alisema pamoja na mambo mengine mpango huo unalenga kuwafikisha watanzania habari sahihi kwa wakati.
Alisema kwa kutambua maendeleo ya teknolojia matumizi ya simu za mkononi katika kutoa taarifa yanazidi kuongezeka na kuwa sehemu ya maisha ya kila siku.
<  Kadiri siku zinavyokwenda teknolojia inaonekana kukua na simu za mkononi kutumika kama njia mojawapo ya kuwasilisha taarifa kutokana na hilo Mwananchi kwa kushirikiana  na Airtel tumekuja na ushirikiano huu ambao utawawezesha wateja wetu kupata taarifa sahihi na kwa wakati > alisema Nanai
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Sunil Colaso  alisema kampuni hiyo imekuwa mstari wa mbele katika kubuni njia mbalimbali zinazorahisisha utoaji wa huduma za mawasiliano na taarifa kwa wateja wake.
Alisema kupitia huduma hiyo watanzania watapata fursa ya kupata habari zinazotokea hapo kwa papo kutoka katika kila kona ya dunia.
Airtel tuko mstari wa mbele kuanzisha huduma ambazo zinalenga kumrahisishia mawasiliano mteja  na kupitia huduma hii ni matumaini yangu watanzania watapata nafasi ya kupata habari mahali popote walipo >alisema Colaso
Alisema kwa kuanzia wateja wa Airtel watapata huduma hiyo bure kwa muda wa siku saba na baada ya hapo watatozwa Sh 120 kwa siku.
 Meneja Masoko wa MCL Bernad Mukasa alisema taarifa zitakazotolewa kwa wateja wa Airtel zitakuwa katika sehemu tatu hivyo mteja atakuwa na uamuzi wa kuchagua habari anazozitaka ambazo zitahusisha habari za kawaida,burudani na michezo.
<  Sasa hivi wateja watakuwa na uamuzi wa kuchagua taarifa wanazohitaji kama ni habari za kawaida,michezo au burudani kwa mujibu wa matakwa ya kila mmoja >alisema Mukasa

Waandishi wa habari wakumbushwa maadili kupitia Daraja Day

$
0
0


Mkuu wa mkoa wa Njombe Kapteni Mstaafu Aseri Msangi amewakumbusha waandishi wa habari kufanya kazi zao kwa kuzingatia maadili ya uandishi wa habari, kwa kuandika habari za uhakika zilizofanyia utafiti wa kina.
Mkuu huyo wa mkoa alitoa ushauri huo alipokuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya miaka minne ya shirika la Daraja, na kutoa wito kwa wanahabari kufanya kazi kwa ufanisi bila kujali wadhifa wa viongozi, na kutowaonea haya viongozi wabovu, wabinafsi, wanaokubatia rushwa na wasiopenda utawala bora na kuwajibika.
 
Wasomaji  wa gazeti la Daraja Letu wakiangalia kilichomo

Simon Mkina akizungumza na umati

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Aseri Msangi akihutubia umati wa Njombe. Sherehe hizo zilikuwa 'live' kwenye radio tatu - Uplands FM, Ice FM na Kitulo FM ili kuwafikia hata wale walioshindwa kufika uwanjani, hasa wakazi wa maeneo ya mbali na Njombe


“Naomba kuwaasa kuwa ni vizuri katika utendaji wa kazi yenu, mzingatie maadili ya uandishi wa habari ili kutoleta mtafaruku baina ya viongozi au serikali na wananchi, hivyo nawashauri kuandika habari za uhakika zilizofanyia utafiti na kujiridhisha,” alisema Msangi.
Alilipongeza shirikala la Daraja kwa kuwa chachu ya maendeleo katika mikoa ya Njombe na Iringa, hasa kupitia gazeti lao la Daraja Letu, kwa kuwafikia wananchi wengi vijijini na kuibua changamoto mbalimbali na hatimaye kuwafuata viongozi ili kutafutia ufumbuzi.
“Naomba kusisitiza gazeti la Daraja Letu liendelee kufanya kazi zake kwa ufanisi bila kujali wadhifa wa viongozi, kutowaonea haya viongozi wabovu, wabinafsi, wanaokumbatia rushwa, wasiowajibika na zaidi wasiopenda utawala bora na kuwajibika,” alisema.
 
Baadhi ya wanajumuia ya Twanga Swali wakiendelea kufuatilia matukio. Hawa ni baadhi ya vijana wanaounda vilabu vya Daraja

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Daraja, Simon Mkina akiwa na baadhi ya watendaji wa gazeti la Daraja Letu. Hawa hutumia zaidi usafiri walionao hapa kusaka habari, kusambaza magazeti maeneo ya vijijiji ambako kuna changamoto kubwa ya miundombinu ya barabara

Msanii kutoka Dar es Salaam, Recho alikuwepo kupamba Daraja Day

Alisema serikali ya Rais Jakaya Kikwete imekuwa ikihimiza ushirikiano baiana ya watendaji wa serikali na vyombo vya habari, na kuahidi serikali yake ya mkoa kutoa ushirikiano wa kutosha kwa wanahabari ili kuhakikisha maendeleo yanayokusudia mkoani hapa yanafanikiwa.
Alitoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Njombe kutumia fursa ya gazeti  hilo kama jukwaa la kufikisha haja zao serikalini kwa kuwaunganisha na viongozi wao kwa kutoa maoni, kueleza kero zao na changamoto mbalimbali zinazowakabili ili zitafutiwe ufumbuzi, huku akiwatahadharisha waandishi kutotumia vyombo vyao kueneza majungu, fitina au uchonganishi bali wawe daraja la kuwaunganisha wananchi na serikali yao ili kudumisha umoja na mshikamano.
Mkurugenzi wa shirika hilo, Simon Mkina alimuomba mkuu huyo wa mkoa kuwahimiza watendaji waliochini yake kuwapa ushirikiano wafanyakazi wa shirika hilo ili wafanye kazi zao kwa ufanisi kwa lengo la kuharakisha maendeleo katika mkoa huo.
Awali mjumbe wa bodi wa shirikala la Daraja Josephine Lemoyan, alisema Daraja ni shirika la kijamii lisilokuwa na kiserikali lisilotengeneza faida, na kuongeza kuwa lengo lake kuu ni kufanya kazi na wananchi na serikali za mitaa kuhimiza huduma bora kwa wananchi kwa wakati na uwazi, na kwamba kwa kipindi cha miaka minne tangu lianze kazi limesaidia kuchochea maendeleo kwa kuhimiza uwajibikaji na utawala bora.

gari lapasuka tairi lagonga daraja na kuua Mwanza

$
0
0


WATU watatu wamefariki dunia na wengine  wanne kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupasuka tairi na kisha kugonga daraja na kupinduka katika kijiji cha Ng’ombe wilayani Misungwi.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, Valentino Mlowola alisema tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 3.40 katika barabara ya Mwanza –Shinyanga.

Aliwataja waliofariki dunia kuwa ni pamoja na Patrick Peter (28) aliyekuwa dereva wa gari hilo, Makoye Nyanda (30) na Hawa Abel(25).
Akifafanua juu ya ajali hiyo, Kamanda Mlowola alisema ajali hiyo ilihusisha gari lenye namba za usajili T 111 BPC lililokuwa likitokea Mabuki kuelekea Mwanza ambapo liligonga daraja na kupinduka .
Aliwataja majeruhi kuwa ni pamoja na  Shija Kabuki (22),Angelina Abel (24), Bune Chenya (40) na Johari Malugu (24)  ambao wamelazwa katika hospitali ya Rufaa ya Bugando kwa matibabu zaidi.

Shakira ataka kuwa na watoto 9

$
0
0


Mtunzi, mwimbaji mzaliwa wa Colombia Shakira Isabel Mebarak Ripoll, ambaye ni maarufu kama Shakira,  ambaye kwa sasa anatamba na  "Can't Remember to Forget You" amesema  ana hamu ya kuwa na watoto 9 na jamaa yake ambaye ni mcheza soka, Gerard Pique.

Mdada huyo ambaye ni dansa,projuza, mrimbwende na kereografa amesema kwamba kinachomzuia kwa sasa ni ratiba yake ya kazi.


Hayo yamo katika jarida la Aprili la mwaka huu la Latina.

"Kama si mambo haya ya muziki, tayari ningeshapata mimba," anasema Shakira mama wa mtoto mwenye umri wa miezi 13.

Mama huyo amesema kwamba anataka kuwa na timu yake ya mpira na bwana wake  Gerard .

Lakini kwa sasa amesema kwamba anafurahia maisha na mtoto wake huyo ambaye alisema anamfanya kwa sasa awe na mawazo yanayolenga zaidi.

Alisema mtoto huyo pia amebadilisha uhusiano wake na wapenzi wake kwa jinsi anavyosikia raha ya kumwelezea mtoto wake alivyo.

Shakira is just as effusive when talking about Pique, her (hunky!) partner of more than three years. "He's with me because he wants to be with Shakira the person, not the celebrity," she says. "There's real love, there's no ulterior motives. And I'm with him because he's the most amazing man I've ever met. We want the same things, we like the same things, we hate the same things. I have never been with someone so passionate in my life."

First Tanzania Diaspora HOMECOMING conference

CHADEMA WAMSAKA MGOMBEA WA CHALINZE

$
0
0

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Chama cha Demokrasiana Maendeleo (CHADEMA) Jimbo la Chalinze kimeanza mchakato wa ndani wa kupata mgombea ubunge kwa ajili ya uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika mapema mwezi Aprili, mwaka huu, ambapo fomu za uteuzi zimeanza kutolewa kwenye Ofisi Jimbo, kuanzia tarehe 4 Machi na mwisho wa kuchukua na kurejesha fomu hizo itakuwa tarehe 7 Machi 2014, saa 10.00, jioni.
Kura za maoni ndani ya chama, zitafanyika tarehe 8 Machi katika Mji wa Chalinze na kufuatiwa na kikao cha kamati ya utendaji ya jimbo ili kufanya uteuzi wa awali kwa mujibu wa Katiba ya chama na hatimaye kikao cha Kamati Kuu kufanya uteuzi wa mwisho ili kupata mgombea atakayeshindana na wagombea wa vyama vingine.
Mpaka sasa wagombea waliochukua fomu kwenye ofisi ya jimbo ni watatu (3) na wagombea wengine watatu (3) wamechukulia fomu Ofisi za Makao Makuu ya Chama, Dar es Salaam, hivyo hadi sasa idadi ya wagombea waliotambuliwa rasmi ni sita.
Tunatumia nafasi hii kuujulisha umma wa Watanzania, hususan wanachama wa CHADEMA, kuwa fomu za kuwania uteuzi wa ndani zinaendelea kupatikana sehemu tatu, Makao Makuu ya Chama, Ofisi ya Jimbo la Chalinze na kwenye tovuti ya chama www.chadema.or.tz

Imetolewa Machi 5, 2014 
Iddi Omary Ucheche
Katibu wa CHADEMA, Jimbo la Chalinze
0756 639014



*TAIFA STARS KUREJEA MCHANA KUTOKA NAMIBIA*

$
0
0
*TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI*



Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inatarajia kurejea nchini kesho
(Machi 7 mwaka huu) kutoka Windhoek, Namibia kwenye mechi ya kirafiki ya
kalenda ya FIFA.

Taifa Stars ambayo katika mechi hiyo dhidi ya Namibia (Brave Warriors)
ilitoka sare ya bao 1-1 itatua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius
Nyerere (JNIA) saa 8.15 mchana kwa ndege ya South Africa Airways.

Timu inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager baada ya kuwasili
itakwenda hoteli ya Accomondia kwa ajili ya chakula cha mchana na baadaye
kuvunja rasmi kambi yake.



*Boniface Wambura Mgoyo*
*Media and Communications Officer*
*Tanzania Football Federation (TFF)*

Sababu za kuwafunga midomo waandishi hazina mashiko

$
0
0



LEO kwa namna ya ajabu kabisa Bunge Maalumu la Katiba limeamua kuwanyima wananchi haki ya kujua kinaendelea nini kwa kuwazuia waandishi kushiriki katika majadiliano ya kamati.
Pamoja na kutoa sababu zao ambazo sisi tunaziona hazina mashiko, kitendo cha kuzuia  mhimili wa 4 katika maisha ya kijamii ni fadhaa kwa wale wanaojua maana na umuhimu   wa wapasha habari.
Pamoja na kupunguza nguvu za usahihi na ukweli, kitendo hicho kitachangia  kuandika habari ambazo zinafurahisha masikio lakini hazina uhakika hasa magazeti pendwa.
Kwa upande wetu tunaona si sahihi kwa Bunge hilo kuzuiwa waandishi wa habari kwa madai kuwa watakosea na kuwapotosha wananchi. Kiukweli kwa kuwazuia hivi ndio wanakuwa na nafasi ya kutafuta ‘umbea’ na kupotosha.
Taarifa watakazopewa waandishi ni taarifa ambazo zitakuwa zimechujwa na kutooneshwa hali halisi ilivyokuwa katika kufikia hitimisho.
Hali ya kunyima haki ya kuandika na kusubiri kukariri taarifa kunaendeleza hali ile ile ya ukimya kwenye haki ya kukusanya na kupasha habari hasa katika matukio muhimu ya kitaifa kama hili la utungwaji wa Katiba mpya.
Mtu yeyote anayejua umuhimu wa wapasha habari kuwepo eneo la tukio kusaidia wananchi kuelewa mwenendo wa shughuli iliyopo mbele yao anapoona anazuiwa atajiuliza swali waheshimiwa hawa wanaogopa nini au wanataka kuficha nini kwani wananchi wana haki ya kujua kinachoendelea.
Tunapaswa tuelewe kuwa zipo sheria na kanuni za ubora wa kazi ya uandishi na waandishi wanaelewa hilo kama wanataaluma ndio maana kama wakiteleza huomba radhi na kama kukiwa na matatizo lipo Baraza lao linasaidia kutatua matatizo yaliyoonekana.
Katika mazingira ya kila mtu anataka kuwapo na uwazi na misimamo kujulikana, kitendo cha kuzuia waandishi kuingia katika kamati hizi muhimu zinazojenga msingi wa majadiliano kwenye Bunge ni dalili ya woga usiokuwa wa lazima.
Ni dhahiri hii Katiba ni ya umma na haihusiani na watawala au wanaotaka kutawala kwa namna yoyote ile, hivyo kitendo hicho cha kunyima fursa hatukishabikii kwa kuwa kinajenga hisia mbaya na msingi mbovu wa kukabiliana  na masuala makubwa ya kitaifa kwa uwazi na bila jazba.

Hoja kwamba bila kamera kuna uhuru wa kuzungumza kunajenga taifa lisilojua linasimamia nini na kujaa uoga usiokuwa na mantiki.
Aidha hoja ya  Mjumbe wa Kamati ya Kanuni George Simbachawene  kwamba kama waandishi wa habari kwenye vikao hivyo wakiruhusiwa habari
zitatofautiana kwa kila mzungumzaji  hiyo ndiyo maana halisi ya kuandika hoja ili kila mwananchi aweze kupima hoja inajengwa namna gani kwanini aje kupiga kura  baadaye.

Aidha madai kuwa waandishi ni wengi kwa hiyo hawatatosha  si msingi kabisa wa kuzungumza kwa tukio kubwa la kitaifa kama hili, kuwepo kwa waandishi wengi ndio kuchanua kwa demokrasia kwani kila mtu atapata haki ya kusoma kwa namna ambavyo waandishi wanachambua kinachoendelea.
Hata injili katika Biblia iliandikwa na watu wanne tofauti lakini wakibeba maudhui yale yale na hata Mungu alibariki.
Wanachotaka watu ni muafaka umefikiwaje na si taarifa ya mwisho, kwani wale ambao wataonekana kutosikilizwa ndio hao watakaotibua kabisa kwani watafikisha yaliyojiri kwa namna yao na waandishi watayaandika.
Kwetu sisi ambao kazi yetu ni daraja kati ya wananchi na watengeneza mustakabali wao sababu zilizotolewa za kuwakataa waandishi katika mikutano ya kamati ni dhaifu.
Tunaamini mchakato wa Katiba haupaswi kuwa
siri , waandishi wanapoaswa kuwa huru katika kuhabarisha umma kwani umma ndio utakaokuja kufanya maamuzi ya Katiba hii.
Ukiangalia kwa makini sababu  zilizotolewa utaona kwamba wajumbe wamejazwa na hofu ambayo haina mantiki.
Tuwaangalie na wenzetu ambao hawakuwa na mpango wa kuchuja habari kwa kuzuia vyombo vya habari wakati waliporekebisha katiba zao, tuwaone Kenya na Afrika Kusini kwani wao waliruhusu waandishi.
Tunaamini hatupo vitani na hatuna sababu za kubadili uhuru wa vyombo vya habari kwani vipo kwa faida ya umma na kuwajengea maarifa ya uamuzi.


JK ATUMA RAMBIRAMBI KWA KIFO CHA SHEIKH WA MKOA WA IRINGA

$
0
0


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425


PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI




Rais wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia Salamu za Rambirambi Mufti wa Tanzania, Sheikh Shaaban Bin Simba kufuatia kifo cha Sheikh wa Mkoa wa Iringa, Alhaj Sheikh Ally Juma Tagalile (96) kilichotokea usiku wa kuamkia tarehe 6 Machi, 2014 katika Hospitali ya Mkoa wa Iringa alikokuwa amelazwa akisumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu.

“Nimeshtushwa, nimesikitishwa na kuhuzunishwa sana kutokana na taarifa za kifo cha Sheikh wa Mkoa wa Iringa, Alhaj Sheikh Ally Juma Tagalile kilichotokea usiku wa kuamkia tarehe 6 Machi, 2014 katika Hospitali ya Mkoa wa Iringa alikokuwa amelazwa kwa matibabu akisumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu”, amesema Rais Kikwete katika Salamu zake.

Rais Kikwete amesema kifo cha Alhaj Sheikh Ally Juma Tagalile  ni pigo kubwa siyo tu kwa Waumini wa Dini ya Kiislamu Mkoani Iringa ambao hakika walikuwa wanamtegemea sana kiuongozi katika masuala ya kiroho, bali pia kwa Waumini wa Dini hiyo kote nchini.

“Natambua kuwa enzi za uhai wake, Marehemu Alhaj Sheikh Ally Juma Tagalile pia alitoa mchango mkubwa katika Utumishi wa Umma hususan katika Sekta ya Afya akiwa na Taaluma ya Udaktari, hivyo kuondoka kwake kumetunyang’nya kama Taifa uzoefu wake mkubwa katika Taaluma ya Afya”, ameongeza kusema Rais Kikwete katika kuomboleza kifo chake.


“Kutokana na msiba huo mkubwa, ninakutumia wewe Mufti wa Tanzania, Sheikh Shaaban Bin Simba Salamu zangu za Rambirambi na pole nyingi kwa kumpoteza mmoja wa Viongozi wa ngazi ya juu wa Dini ya Kiislamu hapa nchini.  Ninamuomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema aipokee na kuilaza Mahala Pema Peponi Roho ya Marehemu, Alhaj Sheikh Ally Juma Tagalile, Amina”, amezidi kusema Rais Kikwete katika kuomboleza kifo cha Marehemu..

Rais Kikwete amemuomba Mufti Sheikh Shaaban Bin Simba kumfikishia Salamu zake za Rambirambi na pole nyingi kwa familia ya Marehemu Alhaj Sheikh Ally Juma Tagalile kwa kupotelewa na Kiongozi na Mhimili muhimu wa familia. Amewaomba wawe na moyo uvumilivu na ujasiri ili wahimili machungu ya kuondokewa na mpendwa wao kwa kutambua kuwa yote ni Mapenzi yake Mola.

Aidha Rais Kikwete ameihakikishia familia ya Marehemu kuwa yuko pamoja nao katika kipindi chote cha kuomboleza kifo cha mpendwa wao kwani msiba huu ni wa wote.  

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

6 Machi, 2014

KWA HILI LAZIMA WAANDISHI WASIWEPO-HALI YA HEWA ILICHAFUKA LEO MCHANA

$
0
0



Semina ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba leo imelazimika kuahairishwa baada ya kuibuka vurugu ndani ya ukumbi wa Bunge. 

Zogo hilo liliumuka baada ya kuibuka kwa mvutano baina ya wajumbe uliosababishwa na kutuhumiana kwamba zipo dalili za upendeleo wanazofanyiwa baadhi ya wajumbe kutokana na sababu za kiitikadi za vyama. 

Hali hiyo ya hewa ilichafuka  baada ya kuibuka kwa mvutano baina ya Mjumbe Mhe. Christopher Ole Sendeka ambaye aliingia katika mvutano na Mjumbe wa Kamati ya Kanuni Mhe Abubakar Hamis Bakari kuhusiana na uwasilishwaji wa majedwali ya marekebisho ya kanuni. 

 Awali Mjumbe Sendeka alipewa ruksa na Mwenyekiti wa muda wa Bunge hilo Mhe Pandu Ameir Kificho,  awasilishe mapendekezo ya mabadiriko katika kifungu cha 58 cha kanuni hizo kilichokuwa kikijadiliwa muda huo. 

 Lakini baada ya Mhe Sendeka kuwasilisha mabadiriko yake, alisimama Mjumbe Bakari ambaye kiutaratibu alipaswa kujibu hoja hiyo hasa kwa kuwa ni mjumbe wa kamati ya kanuni. 

Mhe. Bakari alikataa kupokea hoja ya mabadiriko ya Mhe. Sendeka kwa kusema kuwa hayakuwa yamewasilishwa kwa kufuata taratibu za uwasilishwaji wa mabadiriko ya majedwali, na kwamba Kamati haina mapendekezo hayo hivyo haiwezi kujibu jambo lisilo jadiliwa. 

Katika kukataa huko Bakari alikitupia lawama kiti cha Mwenyekiti huyo kwa madai kuwa kimekuwa kikitaja majina ya wajumbe na kuwapa nafasi ya kuongea wakati hawapo kwenye utaratibu wala hawakuwa wameomba toka awali. 

 Aliongeza kuwa si kwa Mhe. Ole Sendeka pekee, bali pia Mwenyekiti huyo amekuwa akiataja wajumbe wengine wakiwamo Peter Serukamba pamoja na Umy Mwaimu ambao wote hawakuwa wamewasilisha majedwali ya mapendekezo ya marekebisho toka awali. 

 "Mheshimiwa Mwenyekiti, Ole Sendeka hayupo katika orodha ya walioleta mapendekezo, lakini nashangaa wewe unampa nafasi ya kuzungumza wakati hakuwapo kwenye orodha yetu, kamati hatuwezi kumpa nafasi ya kujibu hoja yake hatuitambui. 

"Hata hao wakina Ummy Mwalimu hawapo katika orodha. Mwenyekiti ukiendeleza huu mtindo wa kuruhusu kila anayetaka kuzungumza hapa azungumze hatutofika. tutatumia miezi 6 hapa kutengeza kanuni tu. Lazima uwe na maamuzi kuwa wanaoleta mapendekezo hivi sasa hatupokei"alisema Mhe Bakari 

 Baada ya Mhe Bakari kumaliza kuzungumza, Mhe Kificho aliingilia kati na kusema kuwa jambo hio linaweza kuwa limechanganywa na sekretarieti inayoandaa na kwamba yeye binafsi amepewa majina ya waliopeleka marekebisho hivyo anashangaa kuona kama hayapo kwa wajumbe hao. 

Mhe Kificho alitoa ruksa kwa Ole Sendeka kuongea tena, ambapo katika mazungumzo yake alitoa kaulia akisema kuwa mapendekezo yake aliyawasilisha mapema na kwamba kama Mhe Bakari ana itikadi zake za vyama asimuhusishe humo. 

 Mhe. Ole Sendeka alisema kuwa yeye ana uzoefu wa kanuni na kwamba alifuata taratibu akiwa na wenzakeMhe Serukamba pamoja na Mhe Mwalimu na kwama kama mapigo yao yanawaumiza wajumbe wengine wavumilie tu. 

 "Mheshimiwa mwenyekiti tuliopo hapa ni wajumbe. Nilijua na mimi sio dhaifu kwenye kanuni. Nnajua haki yangu kwa kuwasilisha kwa wakati, nilitimiza wajibu wangu, kama mapigo yetu yanawaumiza. 

 "Kazi yetu si kupeleka majina yetu kwa Abubakari, kama yeye ana chama chake na hoja zetu zinamuuma, asimame na kutuweka wazi kuwa yupo katika msimamo gani. Lakini mimi nimewasiisha kama taratibu zinavyonitaka"alisema Ole Sendeka 

 Kauli ya Mhe Sendeka ilianzisha sintofahamu ndani ya Bunge hilo baada ya baadhi ya wajumbe kuanza kuzomea na wengine wakisiama na kutaka kupewa ruksa ya kuzungumza huku wakiwasha vipaza sauti.

 Hali hiyo ilimuinua Mhe Kificho ambaye aliwasihi wajumbe kuacha kuingiza masuala ya vyama hasa kwakuwa wajumbe walioingia hapo ndani wamewakilisha makundi. 

"Niwaombe wajumbe tujitahidi sana, tusionyeshe misimamo ya vyama, tumepata heshima kubwa ya kuwapo humu ndani hivyo si vyema kuanza kuonesha vidole kwasababu huyu katika CCM, sijui CUF ama Chadema au kokote itaibua hisia ambazo si vyema.

 "Mheshimiwa Ole Sendeka naona ulimi umekwenda mbali kidogo ukamgusa mheshimiwa Bakari. Mimi naona hili jambo limekwenda nje. Kwa hiyo naomba tuwe makini"alisema Kificho

Baada ya kauli ya Kificho, wajumbe walianza kupiga kelele wakitaka Mhe Ole Sendeka kumwomba radhi Mjumbe Bakari huku wengine wakimtaka asifanye hivyo.


Mhe Kificho alitoa nafasi nyingine kwa Mhe Bakari kuzungumza, ambapo katika mazungumzo yake ndipo fujo hizo zilipoibuka.
Katika Mazungumo yake, Mhe Bakari alisema kuwa alichosema yeye ni kwa faida ya Bunge na nchi, na kwamba taratibu ni kuwasilisha mapema mapendekezo na kwamba majina ya kina Sendeka hayakuwapo. 


 "Mimi nilizungumza vizuri hili kuweka utaratibu mzuri wa kupokea majedwali haya. Mheshimiwa mwenyeiti kwa bahati mbaya mdogo wangu Ole Sendeka anadai kanuni anazijua vizuri, lakini ninachosema sifikirii..sifikirii kama ana uzoefu wa kujua kanuni kunishinda mimi.

"Mheshimiwa mwenyekiti toka mwaka 1980 nipo katika mabunge haya, kwa hivyo sifikirii kama mtu katoka Simanjiro miaka kumi iliyopita anaweza akaja hapa na kusema anajua kanuni kunizidi.
"Mimi sitaki aniombe radhi, ila ninachotaka kumfahamisha ni kwamba kuna watu wana ujuzi zaidi kuliko yeye hivyo awe makini katika mazungumzo yake"alisema Bakari 


Kauli hiyo ilizidisha mgawanyiko katika Bunge hilo, ambapo wajumbe walisimama na kuanza kupiga meza wengine wakizomea.  

Baadhi ya wajumbe walionekana wakirushiana maneno na hata kupeleka kutaka kurushiana makonde. 

 Hali hiyo ilipeleka askari ambao ni wapambe wa Bunge kusogea karibu ikiwa ni njia ya kutuliza vurugu hizo, huku wajumbe hao wakiendelea kurushiana maneno. 

 Vurugu hizo zilionekana kusambaa katika ukumbi mzima ambapo wajumbe wengine walionekana kurushiana maneno, hali iliyopelekea Mhe Kificho kuahirisha Semina hiyo.


Jioni mambo yalienda vyema baada ya kauli za kuwekana sawa kutoka mkwa Mbatia na Mwandosya

Source:michuzi blog

POLISI WAPUNGUZA JOTO LA DODOMA;WANASA WATUHUMIWA UKAHABA 15

$
0
0

Na. Sylvester Onesmo wa Jeshi la Polisi Dodoma.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma limeendelea kufanya msako katika maeneo mbalimbali na kufanikiwa kuwakamata wanawake wapatao 15 wanaojihusisha na biashara haramu ya kuuza miili yao kutoka mikoa mbalimbali nchini. Msako huo ulifanyika tarehe 05/02/2014 majira ya 21:00hrs katika mitaa ya uhindini na Air Port.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi DAVID MISIME - SACP amewataja watu hao kuwa ni:
1.   VERONICA D/O JOEL mwenye miaka 23, Mnyakyusa mkazi wa Sai Mbeya.
2.   ROSE D/O MICHAEL mwenye miaka 30, Mgogo, Mkazi wa Kikuyu Dodoma.
3.   MARIAM D/O JORDAN mwenye miaka 26, Mhehe mkazi wa Tukuyu Mbeya.
4.   REHEMA D/O RAMANDANI mwenye miaka 38, Mlugulu makazi wa Airport Morogoro.
5.   JOYCE D/O MARTINE mwenye miaka 22, Mnyamwezi mkazi wa Chinangali West Dodoma.
6.   FATIA D/O SARATIELI mwenye miaka 20, Mgogo mkazi wa Makanda Bahi Dodoma.
7.   BOKE D/O CHACHA mwenye miaka 27, Mkurya mkazi wa Tarime Mara.
8.   SWAUMU D/O BAKARI mwenye miaka 23, Mnyamwezi mkazi Chinangali Dodoma.
9.   ROSS D/O MASAKI mwenye miaka 28, Mchaga mkazi wa Sanya juu Moshi.
10.               SCOLASTIA D/O COSTANTINO mwenye miaka 22, Mnyakyusa mkazi wa Gongolamboto Dar es salaam.
11.               HAPPY D/O JULIUS mwenye miaka 31, Mnyamwezi mkazi wa  Urambo Tabora.
12.               AISHA D/O HASSAN mwenye miaka 38, Mbulu mkazi wa Babati Manyara.
13.               JULIANA D/O DOMINICK Mwenye miaka 31, Mnyakyusa, mkazi wa Airport Dodoma.
14.               DATIVA D/O LUKWEMBE mwenye miaka 29, Mhaya mkazi wa Kiziba Bukoba Kagera.
15.               DORIN D/O MASSAWE mwenye miaka 23, Mchaga mkazi wa Kiboshomaro Moshi.

Aidha Kamanda MISIME amesema katika msako huo watu wawili wanaume walikamatwa wakiwa na mirungi robo kilo katika mtaa wa barabara ya nane (8) Manispaa ya Dodoma ambao ni NASSOR S/O ALLY mwenye miaka 45, Mwarabu mkazi wa barabara ya kumi na AYUBU S/O TEPO mwenye miaka 40, Muarusha, Fundi cherehani mkazi wa Chamwino.
Pia huko katika Wilaya ya Kongwa kijiji cha Mlanje kata ya Matongoro Tarafa ya Zoisa alikamatwa mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la SHEDRACK S/O MACHILE mwenye miaka 46, Mgogo, Mkulima akiwa na Lita 30 za pombe ya moshi akiziuza.

Kamanda MISIME amesema msako unaendelea na amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi.

Jk aenda kumfariji Sophia Simba kwa kufiwa na mtoto

$
0
0
.Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini katika kitabu cha maombolezo
nyumbani kwa Waziri wa Maendeleo ya jamii jinsia na Watoto Mhe.Sophia Simba
kufuatia kifo cha mwanaye Marehemu Leeford Simba huko Mikocheni jijini Dar
es Salaam leo.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji Neema Mathew(kulia) na
waombolezaji wengine kufuatia kifo cha Mumewe Leeford Simba kilichotokea
juzi. Marehemu Leeford Simba ni mtoto wa Waziri wa Maendeleo ya Jamii
jinsia na Watoto Mhe.Sophia Simba.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpa mkono wa pole na kumfariji Waziri
Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto Mhe.Sophia Simba kufuatia kifo cha
Mwanaye Leeford Simba wakati wa ibada ya kumuombea marehemu iliyofanyika
nyumbani kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam leo.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Waziri
Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto Mhe.Sophia Simba alipoenda kumfariji kufuatia kifo cha
Mwanaye Leeford Simba
nyumbani kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam leo.

KAMISHNA JENERALI WA JESHI LA MAGEREZA, AHUDHURIA SHEREHE ZA KUFUNGA MAFUNZO MSUMBIJI

$
0
0
Rais wa Msumbiji, Mhe. Armando Emilio Guaebuza(kulia vazi jeupe) akikagua Gwaride
Maalum lililoandaliwa na Maafisa Magereza Wahitimu wa taaluma ya Uaskari Magereza
Nchini Msumbiji katika Sherehe za kufunga Mafunzo hayo zilizofanyika Machi 07, 2014
katika Chuo cha Maafisa Magereza kilichopo Maputo, Msumbiji ambapo Nchi mbalimbali
za Afrika zilialikwa zikiwemo Afrika Kusini, Zambia, Namibia, Zimbabwe, Swaziland
pamoja na Tanzania. Jumla ya Wahitimu Maafisa 430 wamehitimu vyema mafunzo hayo ya
Uaskari wa Magereza.


Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Tanzania, John Casmir Minja(wa nne toka
kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wakuu wa Vyombo vya
Urekebishaji/Magereza Afrika, Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza Nchini
Msumbiji pamoja Maafisa Magereza Wahitimu wa Kozi namba 08 ya Mwaka 2014 ya taaluma
ya Magereza (upande wa kulia). Wa tano toka kulia ni Kamishna wa Magereza Nchini
Zambia, Percy Chato(wa tano toka kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini
Namibia, Raphael Hamunyela(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

Gadi ya Maafisa Magereza wa Msumbiji Wanaume wakipita kwa mwendo wa haraka wakitoa
heshima mbele ya Mgeni rasmi, Rais wa Msumbiji, Mhe. Armando Emilio Guebuza katika
hafla fupi ya ufungaji Mafunzo ya taaluma ya Uaskari Magereza kwa Maafisa 430 wa
Magereza yaliyofanyika Machi 07, 2014 Maputo, Msumbiji.

Kamishna Jenerali wa Magereza Tanzania, John Casmir Minja akisalimiana kwa kushikana
mikono na Rais wa Msumbiji, Mhe. Armando Emilio Guebuza(kama wanavyoonekana katika
picha) baada ya hafla fupi iliyotanguliwa na Gwaride Maalum katika Sherehe za
kufunga rasmi Mafunzo ya taaluma ya Uaskari Magereza

IKULU YAKANUSHA HABARI ZA GAZETI MWANANCHI YA RAIS KIKWETE KUMTEMBELEA MFUNGWA WA EPA BWANA MARANDA MUHIMBILI

$
0
0
Rais Jakaya Mrisho Kikwete alipotembelea Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Upasuaji wa Mishipa ya Fahamu (MOI) katika  Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jana (Jumamosi) kuwajulia hali wanahabari wawili – Ndugu Salum Mkambala wa Channel Ten (juu) na chini Ndugu Margaret Chambili wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Tanzania yaendelea kuwa kinara wa Utawala bora

$
0
0

   Katibu Mtendaji wa Mpango wa Afrika Kujitathmini Kiutawala Bora (APRM) Tanzania Rehema Twalib (wa kwanza kushoto) akiongea na waandishi wa habari leo jijijni Dar es salaam ambapo Tanzania inaungana na nchi nyingine za Afrika wanachama wa mpango huo kuadhimisha siku APRM na kutoa  taarifa ya tathmini ya utawala bora nchini. Katikati ni Afisa Habari Idara ya Habari MAELEZO Frank Mvungi na wa kwanza kulia ni Mratibu wa APRM Tanzania Dkt. Cuthbert Ngalepeka.



MPANGO wa Afrika wa kujitathmini kiutawala bora (APRM) umebainisha kuwa Tanzania ni moja ya Nchi zinazofanya vizuri katika  utawala bora.
Hayo yamesemwa na Katibu Mtendaji wa APRM Tanzania Rehema Twalib wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam alipokuwa akieleza mafanikio yaliyofikiwa hadi sasa ikiwa ni sehehmu ya maadhimisho ya siku mchako huo ambayo huadhimishwa Machi 9 kila mwaka.
Bi Rehema alibainisha kuwa Tanzania imepata mafanikio katika Nyanja za Demokrasia na Utawala Bora, Siasa, Usimamizi wa uchumi, uendeshaji wa makampuni,Maendeleo ya uchumi-Jamii na Masuala mtambuka kama afya.
Akifafanua zaidi Bi. Rehema alisema Tanzania kupitia APRM imefanya tathmini yake katika maeneo hayo na kuwasilisha ripoti yake mbele ya wakuu wa nchi wanachama na kujadiliwa.
Wakati huo huo alizitaja hatua zinazochukuliwa na Serikali kuwa ni kuanza kufanyia kazi mpango kazi wa kitaifa (NPoA) wa kuondoa changamoto zilizobainishwa katika ripoti ya APRM kuhusu hali ya utawala bora nchini.
Pia Bi Rehema alizitaja hatua nyingine ambazo Tanzania imefikia katikakutekeleza  mchakato wa APRM kuwa ni kuwashirikisha wananchi kutoa maoni yao kuhusu hali ya utawala bora nchini na Serikali kuruhusu wataalamu wa utawala bora kutoka nchi wanachama kuja nchini kuhakiki mchakato huo.
Aidha, Bi Rehema alibainisha kuwa lengo kuu la mpango huu ni kuwashirikisha wananchi ili kushirikiana na Serikali zao kubaini changamoto za utawala bora ili zifanyiwe kazi na kuhimiza nchi kutekeleza viwango vinavyokubalika kimataifa na kikanda.
APRM ni mpango ulioasisiwa machi 9, 2013 na wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika (AU) ambapo Tanzania kwa sasa ni miongoni mwa nchi 34 kati ya 54 za AU zilizokwisha jiunga na mpango huu ambapo ilijiunga mwaka 2004. 
Source:Na Frank Mvungi-MAELEZO

Hawa bodaboda vipi hawa? Waitishia nyau Dola

$
0
0

 
CHAMA cha Waendesha Bodaboda wilaya ya Kinondoni, mkoani Dar es Salaam (CHABOWIKI), kimeiomba serikali kusitisha tamko lake linalopiga marufuku uingizaji bodaboda katikati ya jiji kwa kigezo kwamba agizo hilo litawaathiri kimaisha kutokana na wateja wao wengi kufanya kazi katika maeneo hayo

Hivi karibuni serikali kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) ilitangaza hadharani kuwa ni marufuku kwa bodaboda na bajaji zote Dar es Salaam kuingia katikati ya jiji ifikapo Machi 15, mwaka huu.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, katika mkutano ulioshirikisha zaidi ya wanachama 200, Dar es Salaam jana, wajumbe hao wameomba kukutana kwanza na serikali na kufanya majadiliano ya pamoja kwa minajiri ya kutafuta mbadala wake, kabla ya utekelezaji wa agizo hilo

“Wateja wetu wengi wanafanya kazi katikati ya jiji, sasa kitendo cha kutuambia tuishie Jangwani ni dhahiri kipato chetu kitapungua, na hata hizo bodaboda nazo zitaanza kupungua maana huwezi kufanya kazi isiyokuwa na faida..na mwishowe ajira nyingi zinazotokana na sekta hii isiyo rasmi zitapungua na kupekekea vijana wengi kurudi  vijiweni,” Alisema Mwenyekiti wa CHABOWIKI, Almano Mdede.

Mdede aliongeza kwa kuiomba serikali kuwashirikisha kabla ya kutoa maamuzi yanayowahusu, kwani katika hilo wao wana mawazo mazuri ya namna ya kuhakikisha huduma ya usafiri huo inaendelea kufanyika katika utaratibu unaofaa bila ya kuleta adha yoyote

Kwa upande wake, Katibu wa Chama hicho, George Mbwale, alisema ukiacha wilaya nyingine zilizomo ndani ya mkoa wa  Dar es Salaam, wilaya ya Kinondoni pekee ina vituo vya bodaboda zaidi ya 167 vinavyotambuliwa na serikali, huku vingine zaidi ya 450 vikiwa kutoka wilaya za Temeke na Ilala, hivyo agizo hilo litaathiri zaidi ya vijana 500.

“Huduma ya bodaboda imeleta mapinduzi makubwa katika mustakabali mzuri wa ajira na ustawi wa maisha ya vijana wengi, wakituzuia tusiingie mjini ni sawa na kutuambia rudini vijiweni na mitaani mkaendelee kufanya uhalifu” alisema Mbwale na kuongeza:

“Kama serikali haitatusikiliza, au kama isipotuita kulijadili hili kwa pamoja..au endapo hatutaridhishwa na majibu ya barua tulizowaandikia kuomba kukutana nao kabla ya tarehe ya utekelezaji wa agizo, basi tutatafuta njia ya jinsi tutakavyogomea uchaguzi wa serikali za mitaa na serikali kuu. Na muda mfupi ujao tutatoa tamko la mkoa.”

Mwisho



Viewing all 9274 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>