Quantcast
Channel: Lukwangule Entertainment
Viewing all articles
Browse latest Browse all 9112

AIR BUS ILIVYOTULIA KORONGONI BAADA YA KUUA WANNE NA KUJERUHI 35

$
0
0
Basi la Abiria la  AIR BUS lenye namba za usajili T 106 AGB, likiwa
limepinduka na kutumbukia korongoni kwenye daraja la Mkange , kati ya
Kijiji cha Berega na Kiegeya, wilaya ya Kilosa katika barabara kuu ya
Morogoro- Dodoma , jana asubuhi, kama linavyoonakana.Katika ajali hiyo watu wanne

( Picha kwa hisani ya Mtandao wa Michuzi).
WAKATI Rais Jakaya Kikwete licha ya kuelezea huzuni na masikitiko yake
kufuatia vifo vya watu 39, vilivyotokea katika ajali ya barabarani wilayani
Butiama , Mkoa wa Mara , ajali nyingine mbaya ya AIR Bus imetokea mkoani
Morogoro na kusababisha vifo vya watu wanne na majeruhi wapatao 35.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonard Paul , alithibitisha kutokea
kwa ajali hiyo jana ( Sept 8) majira ya saa 5: 45 asubuhi katika eneo la
Daraja la Mkange kati ya Kijiji cha Berega na Kiegeya , wilayani Kilosa .

Alisema ajali hiyo imepoteza maisha ya watu wanne , wanawake watatu na
mwanaume mmoja ambao walifariki dunia papo hapo , ambao majina hayo
hayaweza kufahamika mara moja , huku wengine 35 kujeruhiwa na
walikimbizwa kwenda
kupatiwa matibabu Hospitali ya Misheni ya Berega.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo, kuwa basi hilo yenye namba za
ujasili T 106 AGB lilikuwa likitokea Dar es Salaam kwenda mkoani Tabora
na kutokana na mwendo kasi liliacha njia na kwenda kutumbukia
korongoni kwenye
daraja la Mkange , lililipo kati ya Kijiji cha Berega na Kiegeya, wilayani
Kilosa kwenye barabara kuu ya Morogoro- Dodoma.

Hata hivyo alisema , baada ya kutokea kwa ajali hiyo dereva wa basi hilo
aliyetambuliwa kwa jina la Bilal Seif alitoweka eneo hilo na Polisi ilianza
msaka ili atiwe nguvuni na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Kwa upande wake Mganga wa zamu wa Hospitali ya Micheni ya Berega , iliyopo
kilometa kadhaa kutoka barabara kuu ya Morogoro- Dodoma katika wilaya ya
Kilosa, Alfred Chiponda , alithitisha kupokea majeruhi hao 35 waliopata
ajali ya basi.

Hata hivyo alisema kati ya majeruhi hao 10 ni wanawake , sita ni watoto na
19 ni wanaumme na baadhi yao wameumia vibaya kwa kuvunjika sehemu
mbalimbali za mwili , wengine kichwani, kuvujika miguu ama mikono.

Kwa mujibu wa Mganga wa Hospitali hiyo , baadhi ya majeruhi walioumia
vibaya wamehamishiwa kwa kupelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa
Morogoro kwa ajili ya matibabu zaidi.

Nao baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo , wakizungumza kwa nyakati tofauti
walidai , dereva wa basi hilo licha ya kuwa katika mwendo kasi ,
pia alikuwa akitaka kulipita gari jingine lililokuwa mbele yake na
kupoteza mwelekeo uliosababisha gari hilo kuacha njia na kupinduka eneo la
darajani. 
Source:John Nditi Habarileo Morogoro 


Viewing all articles
Browse latest Browse all 9112

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>